Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Rais wa Mstaafu wa Marekani Bill Clinton,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake.[Pichana Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Rais wa Mstaafu wa Marekani Bill Clinton,(katikati)
aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe wake,(kushoto) Chalsea
Clinton,ni Mtoto wa Rais Mstaafu wa Marekani.[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifuatana na Rais wa Mstaafu wa Marekani Bill Clinton,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar baada ya mazungumzo yao leo.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Mtoto
wa Rais Mstaafu wa Marekani Chalsea Clinton,akipiga mpira kama ishara
ya kufungua mpambano wa Timu za wachezaji wa zamani katika sherehe za
Ziara ya Rais wa Mstaafu wa Marekani Bill Clinton,kukagua miradi mbli
mbali katika nchi za Afrika iliyo chini ya ufadhili wa Taasisi yake,(CLINTON FOUNDATION) katika uwanja wa Amaan leo.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mtoto wa Rais Mstaafu wa Marekani Chalsea
Clinton,baada ya kufungua mpambano wa Mpira wa Miguu kwa timu za
Wachezaji wa Zamani uliofanyika leo katika Uwanja wa Amaan ,(katikati)
Rais wa Mstaafu wa Marekani Bill Clinton,[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
Wasiosikia wafarijika kwa kuhudumiwa na watu Mashuhuri
Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akifurahia jambo alipokuwa
akimskiliza kutoka kwa Mkurugenzi wa Montage Bi Teddy Mapunda mara baada
ya kuwasili katika eneo ambapo kulikuwa kunatolewa huduma ya vifaa vya
kusaidia usikivu jana jijini Dar es Salaam. Huduma hii ya kijamii ya
kusaidia watu wenye matatizo ya kusikia imekuwa ukitolewa kwa
ushirikiano wa taasisi za Starkey ya Marekani, Montage ya Tanzania na
Serena Hotel ambapo hii ni mara ya tatu tokea wameanza kutoa huduma
hiyo.
Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akimuwekea kifaa cha kusaidia
usikivu mwanafunzi aliyetambulika kwa jina moja la Adrian ambaye jana
jijini Dar es Salaam.Huduma hii ya kijamii ya kusiadia watu wenye
matatizo ya kusikia imekuwa ukitolewa kwa ushirikiano wa taasisi za
Starkey ya Marekani, Montage ya Tanzania na Serena Hotel ambapo hii ni
mara ya tatu tokea wameanza kutoa huduma hiyo.
Mchezaji
wa Kimataifa wa Mpira wa Kikapu anayecheza ligi ya NBA nchini Marekani
Hasheem Thabeet akiwa na mwanzilishi ambaye pia ni Daktari bingwa wa
magonjwa ya usikivu William Austin alipotenmbelea kliniki ya kuhudumia
wagonjwa wenye matatizo ya usikivu hapa nchini iliyoratibiwa na Taasisi
ya kusaidia usikivu (Starkey) kwa kushirikiana na kampuni ya Montage ya
Tanzania na Serena Hotel jana jijini Dar es Salaam.
Mchezaji
wa Kimataifa wa Mpira wa Kikapu anayecheza ligi ya NBA nchini Marekani
Hasheem Thabeet akimpa mazoezi ya kusikia mmoja wa wagonjwa
alipotenmbele eneo ilipokuwa inatumika kwa ajili ya kliniki ya kuhudumia
wagonjwa wenye matatizo ya uskivu hapa nchini iliyoratibiwa na Taasisi
ya kusaidia usikivu (Starkey) kwa kushirikiana na kampuni ya Montage ya
Tanzania na Serena Hotel jana jijini Dar es salaam
Mwanzilishi
wa StarKey taasisi ya kusaidia usikivu ambaye pia ni Daktari bingwa wa
magonjwa ya usikivu William Austin mwenye fulana ya bluu akifuatilia
maendeleo ya mgonjwa wa usikivu wakati akipewa mazoezi nkufuatia
kupatiwa kifaa cha kumsaidia kusikia jana jijini Dar es Salaam..
Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa wa pili kushoto katika picha ya
pamoja na waratibu wa kliniki ya kuhudumia watu wenye matatizo ya
kutosikia alipotembelea kliniki hiyo jana jijini Dar es Salaam.Kutoka
kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Starkey Judith Robert, Mkurugenzi wa
Montage Teddy Mapunda na Mkurugenzi wa Masoko wa Serena Hotel Serafin
Lusala.
Picha zote na Frank Shija – MAELEZO
0 Comments