Random Posts

STRABAG KWACHAFUKA

 Meneja Mradi wa ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo haraka wa Kampuni ya STRABAG,Bw FRANK ROHDE kuhusu malalamiko juu ya wafanyakazi kuhusiana na mishaara yao
 Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam akipokelewa na baadhi ya wafanyakazi baada ya kuwasiri ktk ofisi za STRABAG maeneo ya ubungo
 Wafanyakazi wakiwa wamebeba mabango yaliyo andikwa ujumbe wa aina mbalimbali.
 Mhe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki akiongea na wafanyakazi mara baada ya kuwasili hapo
 Bwana fedha wa kampuni hiyo,Ahmed Nasimu ambaye miongoni wa vyiongozi wanaolalamikiwa
 Mhe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki akiongea na baadhi ya viongozi wa kamati ya usala ya ubungo
 Mwasibu ,Bw Snton Nghumbi akiwa chini ya ulinzi akipelekwa kituoni kwaajili mahojiano.
 Wafanyakazi wa Kampuni hiyo wakimsiliza Katibu wa TAMICO Kanda ya Dar se salaa na Pwani,Bw Chales Mgashi,

 
 Daraja likiwa maeneo ya Ubungo likiwa limesimama kwa ujenzi
Mhe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki akiongea na  vyombo habari mbalimbali mara baada yakumaliza kikao cha dharula.kati ya uongozi na chama cha wafanyakazi (TAMICO)
(PICHA ZOTE NA BERNARD JAMES WA MTAZAMO MEDIA DAR ES SALAAM) 
...............................................................................
Na Bernared James Mtazamo Media Dar es salaam

Wafanyakazi wa kampuni ya kimataifa ya ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo haraka,jijini Dar  es salaam wameugomea uongozi wao wakishinikiza kulipwa mishahara na marupurupu yao yote wanayo stahihi kulipwa,pia wameulalamikia uongozi wao kwa kutowajali na kuwabagua wazawa .huku ukiwapendelea wageni ambao ni wa Kenya na Wahindi.ambao wanalipwa pesa nyingi sana tofauti na wazawa wakati wanafanya kazi zinazo fanana,pia wamelaani kitendo chakuwalipa sh,mia saba 7 ya chakula kwa siku hii nidhihaka kwa wafanyakazi,pia wameiomba serikali kupitia Wizara ya mambo ya  Ndani kuchunguza kwa kina maana kuna wageni wengi wanafanya kazi bila vibli,na hata wenye vibali wanafanyakazi ambazo watanzania wapo wanaoweza kuzifanya  huu ni unyang’anyi wa wageni kuchukua kazi zetu,Tanzania inazalisha  wanachuo wengi wanaomaliza vyuo vikuu ambao wanakosa kazi nakupewa wageni alisikika mfanyakazi mmoja akilalamika.kabla ya hapo meneja wa mradi(project manager)FRANK ROHDE alijaribu kuzuia wawndishi wa habari kuingia ndani  akisisitiza kwamba hakuna tatizo lolote lile kitu kilichofanya wafanyakazi kumjia juu ukuwakitishia kumpiga hivyo kunywea nakuachia waandishi waingie,Baada ya wafanyakazi kutoa malalamiko yao ambayo ni mshahara.na marupurupu,vitendea kazi,manyanyaso,baada yakusikiliza malalamiko yao waandishi waliamua kusikiliza upande wapili2,yaani uongozi’baada ya kumfata meneja mradi MR F RANK aligoma kuongea chochote huku akisema kumetokea wizi asuhi ile nakwamba wamevamiwa na majambazi ambayo yamevunja sefe ya pesa nakutokomea nazo,baada yakumteka mhasibu anayejulikana kwa jina la SANTON JOSHUA NG’HUMBI  kasha kumnyang’anya funnguo ambazo walizitumia kuingia nazo ndani ya chumba wanamohifadhia fedha ,kitu ambacho kilipingwa vikali na walinzi walio kuwa zamu,nakusema hakuna kitu kama hicho kilicho tokea hizo ni mbinu za kitoto zinazofanywa na uongozi/FRANK alipobanwa zaidi na waandishi.aliwaomba wasimpige picha na anaomba wakutane faragha ili awape kahawa.

Post a Comment

0 Comments