Na Bernard James
Dar es Salaam
MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi
(UVCCM), Sadifa Juma Khamis amesema kila Mwanachama ana wajibu wakumsimamia
mgombea anaeteuliwa na chama katika uchaguzi wa nafasi mbalimbali ikiwamo
uraisi.
Amesma kutokana na hali ni vyema kila mwana CCM ahakikishe
natekeleza suala hilo kwa umakini kwa kuchagua mtu ambye atakuwa na manufaa kwa
chama na wananchi kwenye majimbo yao.
Kauli hiyo alitoa Dar es salaam juzi katika ziara yake ya
siku mbili katika Wilaya ya Kinondoni.
Alisema kutokana na hali hiyo hivi sasa kila mwanachama
anatakiwa kuwapima wagombea wa nafasi za udiwani na ubunge kama wana sifa za
kutosha kabla ya kufanya uwamuzi kwa vile kufanya hivyo kutakifanya chama hicho
kushinda uchaguzi wa mwaka 2015.
“Mgombea atakayechaguliwa na wana CCM ndiyo atakuwa huyo
huyo nasi tutapambana kuhakikisha
anashinda uchaguzi kwa kumnadi kwa wananchi.
“Ni kwa hapa mna fursa ya kujiandaa sasa na si vinginevyo na
kila kijana ahakikishe kuwa jimbo hili linarejea katika mikono ya CCM kwa
sababu sie ndiye tuliosababisha mbunge wa sasa kushinda kutokana na hali ya
makundi ndani ya chama chetu,alisema Khamis.
Msanii Babu naye akitoa burudani
Wanachama wa CCM wakijimwaga uwanjani
0 Comments