Random Posts

WAZAWA WAPEWE KIPAUMBELE KATIKA UMILIKI VITALU VYA GESI NA MAFUTA NCHINI






 
Eric Mashauri Mkurugenzi Kampuni ya kizalendo Travel Patner akiongea na waandishi wa Habari 

Na Bernard  James

SERIKALI imetakiwa kutoa kipaumbele kwa wawekezaji wazawa kwenye sekta ya mafuta na gesi kwa kuwa walio wengi wanauwezo,mitaji na elimu hiyo jambo litakalosaidia kuinua uchumi wan chi na wa mwananchi mmoja mmoja.

Pia,wawekezaji hao wazawa,wamelaani kauli iliyotolewa hivi karibuni na Waziri wa Nishati na Madini,Prof.Sospiter Muhongo iliyoonekana imewadhalilisha wazawa kwa kuwaambia kuwa hawana mitaji ya kuwekeza kwenye sekta hiyo inayokuwa kwa kasi hivi sasa nchini.

Akizungumza kwenye mkutano wa pili wa wadau wa mafuta na gesi uliomalizika jana jijini Dar es salaam na kushirikisha wadau kutoka mataifa mbalimbali,Mkurugenzi wa kampuni ya huduma za mafuta na gesi ya JAR,Erick Mashauri,alisema hivi sasa wazawa wamejipanga ili kuhakikisha sekta hiyo inawanufaisha waTanzania badala ya kuwa laana.

Mashauri aliishauri serikali kuhakikisha inaboresha mazingira ya uwekezaji ili kuepuka madhara makubwa kama yakiyotokea kwenye sekta ya madini ambapo wananchi walio wengi hawanufaiki na uwekezaji huo hivyo kuzidisha migogoro baina ya pande hizo mbili.

Mwekezaji huyo ambaye pia anajishughulisha na sekta ya utalii kwa kukodisha magari na kukambika,inamilikiwa kwa asilimia mia moja na wazawa huku ikiwa imeajiri wafanyakazi zaidi ya 70 hivyo kuwa ni moja ya kampuni zenye kuleta tija kwa kuhakikisha uchumi wan chi unakuwa.

“Utafiti na uchimbaji mafuta na gesi unaweza kufanyika na kuisha lakini inapaswa tujiulize,wananchi wamefaidika vipi na uwekezaji huo?Naomba tuhakikishe uwekezaji huo unakuza pato la mtanzania kwa kuwa Tanzania siyo masikini kama tunavyodhani”,alisema Mashauri.

Aliongeza kuwa,”kama tukiendeleza dhana ya kuwaona wawekezaji toka nchi za nje kuwa ndiyo wenye uwezo na mitaji ya kuwekeza,tutashangaa nchi zao zinazidi kutajirika huku sisi tukilazimika kwenda kuomba misaada ambayo mara nyingi huja na masharti mengi na magumu lakini wakati umefika sasa kuwaamini wazawa kuwa nao wanaweza”.

Aidha,kampuni hiyo tayari imekwisha wekeza zaidi ya dola za Marekani milioni 300 kwenye sekta hiyo hivyo hakuna haja ya kuwaona watanzania kama masikini wasiokuwa na mitaji mikubwa.

Alitolea mifano ya baadhi ya huduma ambazo serikali inatakiwa kuwapatia wazawa wazitekeleze kuwa ni pamoja na huduma za usafi,upishi,ufundi na za mahusiano ambazo zote wanaweza kuzifanya wazawa.

“Utashangaa mafundi magari wanatoka nje ya nchi,wafanya usafi na hata wapishi,jamani hivi kweli sisi hatuwezi kupika au kurekebisha magari?Naiomba serikali hii ihakikishe  inaorodhesha shughuli zote ambazo zitafanywa na wageni na zile za wazawa ili kuondoa migogoro isiyokuwa ya maana”.

Wakati ombi hilo likitolewa na Mkurugenzi huyo,hali halisi inaonesha kuwa nwazawa wengi hawaaminiki kupewa miradi mikubwa ya uwekezaji kwani wakati wa michakato ya kuuzwa kwa baadhi ya mashirika ya umma wengi wao waliomba lakini hawakupata hivyo kuwavunja moyo wa biashara ya ushindani ikiwa ni pamoja na kutoaminika kwenye uwekezaji wa kimataifa.
mwisho

Post a Comment

0 Comments