Random Posts

MKUU WA MKOA WA DODOMA AONGOZA MATEMBEZI YA WIKI YA MAJI DODOMA MACHI 15, 2014



Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi (kushoto), akikata utepe kufungua matembezi kwa ajili ya maji, yaliolenga kuihamasisha jamii kuhusu utunzaji wa miundombinu ya maji nchini.yaliofanyika katika kata ya Chibelela wilayani Bahi  Machi 15, 2014 (katikati), ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Betty Mkwasa, na kulia Mwenyekiti wa Kijiji cha Chibelela, Dorice Mkwawa.

PICHA  KWA HISANI  YA  PHILEMON SOLOMON  WA  FULLSHANGWE  DODOMA


Kikundi cha ngoma ya asili ya Kigogo kikitoa burudani kabla yakuanza matembezi kwaajili ya kuihamasisha jamii kuhusu utunzaji wa miundombinu ya maji nchini.yaliofanyika katika kata ya CHIBELELA wilayani BAHI  Machi 15, 2014

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Chibelela Bahi wakiwa wamejipanga kumpokea mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi.

 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Chibelela Bahi wakiwa tayari kuongoza maandamano.

Watatu kulia, ni Katibu wa CCM Tawi la Chibelela Bahi, Tito Lusinde akiwa pamoja na viongozi wengine wakiwa wamejipanga kumpokea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi.

Wakazi wa kata ya Chibelela wilayani Bahi nao wakiwa tayari kumpokea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi.


Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Betty Mkwasa akipanda Mti wakati wa matembezi hao.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi.akipanda Mti wakati wa matembezi kwa ajili ya maji, yakilenga kuihamasisha jamii kuhusu utunzaji wa miundombinu ya maji nchini.matembezi hao yalifanyika katika kata ya Chibelela wilayani Bahi  Machi 15, 2014.

Wanafuzi wa Shule ya Msingi Chibelela wakiwa wamesimama na mabango yenye ujumbe mbalimbali.

Kushoto. Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi, Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Betty Mkwasa, pamoja na viongozi wengine wakiwa kwenye matembezi kwa ajili ya maji, yakilenga kuihamasisha jamii kuhusu utunzaji wa miundombinu ya maji nchini. yaliofanyika katika kata ya Chibelela wilayani Bahi  Machi 15, 2014

Mwakilishi kutoka Water Aid, Herbat Kashililah akisisitiza jambo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi akihutubia wakati wa matembezi kwa ajili ya maji, yaliolenga kuihamasisha jamii kuhusu utunzaji wa miundombinu ya maji nchini. yaliofanyika katika kata ya Chibelela wilayani Bahi  Machi 15, 2014.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Chibelela wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi wakati akitoa hotuba yake.

Post a Comment

0 Comments