HABARI PICHA-NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE DAR ES SALAAM
Kampuni ya Smile communications Tanzania (Smile), inayotoa huduma ya intaneti Dar es Salaam na Arusha, leo imeendesha droo ya mwisho katika droo za wiki kuhitimisha promosheni ya “Shinda iPad” ambapo wateja 13 washindi wa droo hiyo wamejinyakulia iPad kila mmoja.
Katika ofa hiyo, wateja wapya wa Smile walitakiwa kununua kifaa cha Mi-Fi au Router kutoka katika maduka au vibanda vya Smile ndani ya mwezi Machi ili kupata nafasi ya kushindania moja kati ya iPad 13 zilizokuwa zikishindaniwa.
Promosheni hiyo iliyokuwa ikisimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha (TGB) imewazawadia wateja tisa (9) kutoka Dar es salaam na (4) kutoka Arusha.
Droo ya mwisho imefanyika leo makao makuu ya Smile Dar es Salaam ambapo washindi wanne wa mwisho wamechaguliwa.
Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa Masoko wa kampuni hiyo Linda Chiza, amesema kampuni yake imetoa zawadi ya toleo jipya la iPad lililowezeshwa katika teknolojia ya 4GLTE zikiwa na vivurushi vya GB5 za intaneti.
“ Tunawapongeza washindi na wote walioshiriki na kutembelea kwenye sehemu tunazotolea huduma” alise Chiza na kuongeza kuwa “ kila mwezi tunakuwa na kitu cha kuwafanya watabasamu. Tutawajulisha nini kinafuata”.