Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akikaribishwa kwenye kituo cha walemavu cha
Rasibura na Ndugu Simon Mnimbo, Mkurugenzi wa Shirika la Caritas la
Kanisa Katoliki Jimbo la Lindi wakati Mama Salma alipokitembelea kituo
hicho tarehe 20.4.2014, siku ya Pasaka kwa ajili ya kuwapelekea zawadi
za sikukuu.
Jengo
linalotumika kwa makazi ya walemavu huko Rasibura, katika Mji wa Lindi
likiwa katika hali mbaya ya uchakavu. Jengo hilo awali lilikuwa
likitumiwa kama gereza na Jeshi la Magereza la Lindi na baadaye
kukabidhiwa kwa Idara ya Ustawi wa Jamii na ndipo walipoamua kutumia
kama jengo la kuwatunzia watu wenye ulemavu.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akitembelea sehemu mbalimbali za jengo la
kuwatunzia walemavu huko Rasibura Mjini Lindi akiongozwa na Mlezi wa
Kituo hicho Ndugu Simon Mnimbo kutoka Kanisa Katoliki Jimbo la Lindi
tarehe 20.4.2014.
Mke
wa Rais, Mama Salma Kikwete akiongea na watu wenye ulemavu mbalimbali
wanaoishi Rasibura baada ya kutembelea sehemu mbalimali za jengo lao.
Mama Salma aliwatembelea walemavu hao wakati wa sikukuu ya pasaka na
kuwapa zawadi mbalimbali za sikukuu hiyo tarehe 20.4.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na mtoto Idd Mohamed Chitawala ambaye ni mlemavu wa macho anayeishi katika kituo cha rasibura pamoja na Baba yake Mzazi Bwana Mohamed Chitawala.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkabidhi Kiongozi wa Kituo cha walemavu cha Raisbura Bwana Mohamed Chitawala baadhi ya vyakula alivyowaletea- mchele, unga, mafuta ya kupikia, sukai, soda na vinginevyo wakati alipotembelea kituo cha walemavu cha Rasibura huko Lindi siku ya Pasaka tarehe 20.4.2014.
Picha na John Lukuwi