Gari iliyobeba Mwili wa marehemu Chill Challa likiwasili Nyumbani kwa marehemu
Ndugu na Jamaa wakishusha Mwili wa marehemu Chili Challa
Mwili wa Marehemu ukishushwa kwa ajili ya ibada
Mke wa marehemu akiwa na majonzi
Ndugu wa Marehemu wakiweka Shada la maua
Mpiga
Gita mahiri wa bendi ya Skylight Chill challa amezikwa jana kwenye
makaburi ya Mwananyamala kwa kopa na mamia ya watu na wanamuziki
wenzie.Marehemu Chill challa alifariki Tar 17-04-2014 hospitali ya Taifa
ya Muhimbili.Chanzo cha kifo cha marehemu ni shinikizo la damu ambapo
kabla ya kifo chake alikuwa katika afya njema,lakini Usiku wa Tar 16
marehemu alidondoka gafla bafuni na ndipo alipkimbizwa hospitalini.
Madaktari walijitaidi kwa kila hali na mali kuokoa uhai wa marehemu
lakini ilishindikana kutokana na shinikzo la damu kuwa kubwa sana na
ndipo Chill challa akafariki dunia,Marehemu Chill challa ameacha Mke na
watoto wawili,Marehemu alikuwa ni mpiga gita mzoefu na mahiri ambaye
amepitia karibu bendi zote kubwa na kongwe nchini kama Akudo,Fm academia
Nk.
uongozi mzima wa Skylight band unawashukuru wale wote waliojitoa kwenye msiba huu na Mungu awabariki.
PICHA ZOTE NA DJ SEK BLOG