Random Posts

PIGO KWA MUZIKI TANZANIA: MUHIDIN GURUMO AFARIKI DUNIA


Na Saidy Mdoe, Dar es Salaam
MWANAMUZIKI mkongwe mwenye historia ya kipekee katika muziki wa Tanzania, Muhidin Maalim Gurumo amefariki dunia leo saa 9 mchana.
Habari kutoka ndani ya familia ya Mzee Gurumo zimeiambia Saluti5 kuwa mwimbaji huyo amefariki katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Kwamba jana usiku Gurumo aliugua ghafla na kukimbizwa Muhimbili kabla mauti kumkuta leo mchana. Taarifa hizo zinasema Gurumo alikuwa akilalamika moyo kumuuma.
Pumzika kwa amani; Mzee Muhiddi nGurumo enzi za uhai wake
Gurumo alizaliwa mwaka 1940 na historia yake kimuziki ikaanzia mwaka 1960 kupitia bendi Kilimanjaro Chacha kabla ya kujiunga Rufiji Jazz Band mwaka 1962.
KUSOMA ZAIDI KWA HISANI YA TOVUTI YA  SALUTI 5 BOFYA HAPA CHINI