Random Posts

RAIS WA LIBERIA AIANGUKIA MAREKANI KUSAIDIA NCHI YAKE KUTOKOMEZA EBOLA



MONROVIA-Liberia watu wengi wameambukizwa virusi vya ugonjwa wa Ebola na wengi wao wapo katika hali mbaya,magari ya wagonjwa ambulance yamekuwa yakichukua wagonjwa na kuwapeleka katika zahanati za katikati,
Hali ni mbaya na imemlazimu Rais kuiomba Marekani itume vikosi ya matibabu ilikukabiliana na ugonjwa wa Ebola ambao unatishia uhai wa wariberia na kuliteketeza Taifa.Rais anasema misaada zaidi inahitajika ,Rais Ellen Johnson Sirleaf  jumatano hii ameiomba jumuiya ya kimataifa kuzidisha misaada mala 2 ilikukabiliana na ugonjwa huu,ambao unaenea kwa kasi sana.
Kuna hatari ugojwa wa ebola kusambaa katika mataifa mengine za  Afrika,baada ya kuwa tayari umeisha shambulia mataifa matano ya Afrika magharibi.
Marekani ni wenzetu hapa Liberia,atuwezi peke yetu katika kuutokomeza ugonjwa huu alisema Sirleaf katika taarifa yake iliyosomwa,tunatumaini uamuzi wa Marekani utachochea  jamii ya kimataifa  kuchukua hatua  ya kuungana ilikuutokomeza ugonjwa wa ebola,wafanyakazi wengi wa afya waliokuwa wanahudumia wagonjwa ,wengi wao wamegunduliwa kuambukizwa ,katika nchi za Guinea,Liberia na Siera leoni nusu yao tayari wamekufa,pia wafanyakazi wa afya kutoka ulaya walioenda kusaidia ambao wako saba wamegundulika kuwa na vijidudu vya ebola na tayali wamepelekwa katika nchi za ulaya kwa matibabu wakiwa chini ya uangalizi,
Imekuwa vigumu sasa kuwapa mafunzo wahudumu wengine wa afya kwa ajili ya kwenda kutoa hudma katika nchi hizo kutokana na maambukizi yalivyo.,kunamlipuko mkubwa wa ugonjwa wa ebola.