Na Bernard James 0652152000
Jukwaa la katiba Tanzania
(Jukata)limemtangaza Mhe Samweli Sitta ambae ni mbunge wa jimbo la urambo na
Spika wa bunge maalumu la kuandika katiba mpya ,pamoja na Mwanasheria mkuu wa
Serikali jaji Warema kuwa ni maadui wakubwa wa upatikanaji wa katiba bora ya
Tanzania,
Akizungumza na waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam Mwenyekiti
wa jukata ,Deus M Kibamba alisema
Mwanasheria mkuu wa serikali na Sitta wanawapotosha kwa makusudi wabunge wa
waliopo Dodoma kuwa katiba mpya itapatikana hata bila kuwepo Ukawa,na mwanasheria
mkuu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakati wanajuwa haiwezekani ,Kupatikana
katiba bila malidhiano,Kibamba a lienda mbali zaidi na kusema kuendelea kwa
mchakato Dodoma kwasasa ni ufujaji wa pesa za waTanzania walipakodi kwa manufaa
binafisi sio kwa ajili ya manufaa ya wa Tanzania,ameshauli kusitishwa kwa bunge
mala moja ,
Jukwaa la katiba la Tanzania
lilipokea kwa furaha tamko la vyama vya siasa lililotokana na makubaliano
yaliofikiwa kwenye mkutano kati ya vyama vya siasa vilivyo chini ya kituo cha
Demokrasia Tanzania (TCD)na Mhe Rais iliyofanyika tarehe30/8/2014 na 8/9/2014
ikulu ndogo ya chamwino Dodoma,kutokana na mazungumzo hayo,ilikubaliwa mchakato
wa katiba mpya uairishwe hadi baada ya
uchaguzi wa 2015
Deus alisema Bunge maalum la
katiba (bmk)limekosa uhalali wa kisiasa kutokana na kutoka nje ya bunge kwa
kundi la UKAWA na mahudhulio duni kutokana na mahudhulio duni kutokana na
wabunge 25 wa CCM kutoshiriki vikaotangu bunge lilipoanza Agosti05/2014
Bunge pia limekosa uhalali wa
kisheria itakapo kuja kwenye kupata2/3 kutoka Zanzibar wakati wakupigia kura
vifungu na ibara mbalimbali za katiba,kwa hiyo kuendelea na bunge la katiba ni kuendeleza wizi wa mabilioni ya waTanzania na
ufujaji na kufuru ya matumizi ya fedha za umma za walipakodi waTanzania ambao
ni masikini.kujiengua kwa mwanasheria
mkuu wa Zanzibar Mheshimiwa Othumani Masoud Othumani kutoka katika
kamati ya uandishi ya bunge maalum la katiba kumekuwa ni pigo kubwa kwa
mchakato wa katiba mpya na hususani bunge maalum .habari ya kuwa kuondoka kwa
mwanasheria mkuu wa serikali ya mapinduzi Zanzibar hakuna pengo lolote kama
Sitta na Warema wanavyotaka kuaminisha jamii,ni propaganda na upotoshaji
unaostahili kupuuzwa ikizingatiwa kuwa mwanasheria mkuu wa Zanzibar ndie
kiongozi wa jopo la waandishi na wanasheria
kutoka upande wa Zanzibar na mshauri mkuu wa sheria wa SMZ.kwa hiyo kujiengua kwake ni
pigo kubwa na athali kwa
maslai ya Zanzibar,Deus Kibamba
amewaomba waTanzania kwa ujumla wake kumuona Mhe Samweli Sitta na Mwanasheria
wa Serikali Jaji Warema kuwa ni maadui wakubwa katika kupatikana kwa katiba
bora kwa masilai ya Tanzania na vizazi vijavyo,kwa hiyo wasipewe nafasi
yeyote katika chaguzi zijazo kwa muda wa
miaka kumi 10 iliwajirudi,na mchakato unaoendelea hivi sasa kule Dodoma ni
masilahi binafisi, na usitishwe malamoja alisema mwenyekiti Deus
