Random Posts

WATANZANIA WAASWA KUWA WA MOJA KWENYE UJENZI WA NCHI.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiongea leo na wakazi wa Dodoma na watanzania kwa ujumla wakati wa shughuli ya maadhimisho ya Siku ya kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania na kuwaasa watanzania kudumisha amani ambayo ilipatikana baada ya Mashujaa wetu kuipigania na hata kujitoa uhai wao kwa ajili ya Taifa.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili  Mheshimiwa Alhaji Ali Hassan Mwinyi akiongea leo na wakazi wa Dodoma na watanzania kwa ujumla wakati wa shughuli ya maadhimisho ya Siku ya kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania na kuwataka watanzania kumuunga mkono Mhe. Rais Dkt. Magufuli katika harakati za kuijenga Tanzania mpya.

Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa  Dkt.Ali Mohamedi Shein akiongea leo na wakazi wa Dodoma na watanzania kwa ujumla wakati wa shughuli ya maadhimisho ya Siku ya kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania na kusisitiza kuhusu umuhimu wa watanzania kuenzi amani iliyoasisiwa na wazee wetu na kuacha kushiriki katika vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani.

Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa John Samweli Malechela akiongea leo na wakazi wa Dodoma na watanzania kwa ujumla wakati wa shughuli ya maadhimisho ya Siku ya kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania na kumshukuru kwa kusimamia na kutekeleza ahadi zilizowahi kutolewa na hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikiwemo kuhamishia serikali Mkoani Dodoma.