Random Posts

WACHEZAJI SIMBA WAIFANYIA KWELI AZAM FC HUKU WAKIMKUMBUKA KIPENZI CHA TIMU HIYO MAREHEMU PATRICK MAFISANGO


Mchezaji wa Simba  Shiza Kichuya akishangilia huku akiwa amebebwa na Laudit Mavugo mara baada ya kuifungia    timu yake ya Simba goli katika dakika ya 67 kwenye kipindi cha pili cha mchezo wa ligi kuu ya Vodacom katika  uwanja wa Uhuru wakati Simba ilipocheza na timu  ya Azam FC  Jumamosi septemba 17, 2016jijini Dar es salaam , Katika mchezo huo Simba imetoka kifua mbele  kwa kuibuka na ushindi wa goli  1-0 dhidi ya Azam FC


Wachezaji hao Walishangilia goli lao na kukimbilia mbele ya bango la picha ya mchezaji aliyekuwa kipenzi cha mashabiki wa timu hiyo Marehemu Patrick Mafisango aliyepoteza maisha kwa ajali ya gari jijini Dar es salaam na kusafirishwa nchini kwao DRC Congo, ambako alipumzishwa  katika nyumba yake ya milele akiwaachia majonzi makubwa mashabiki wa Simba  kutokana na umahiri wake katika kucheza mpira ambao uliisaidia na kuipa mafanikio klabu hiyo.
Mchezaji wa Simba  Laudit Mavugo akishangilia na wenzake mbele ya picha ya Marehemu Patrick Mafisango aliyekuwa mchezaji mahiri wa timu hiyo kama kumbukumbu yake katika mchezo uliochezwa  kwenye uwanja wa Uhuru huku Simba ikiibuka na ushindi wa Goli 1-0 dhidi ya Azam FC.
Mchezaji Ibrahim Ajib wa Simba akichuana vikali na Mchezaji Brce Kangwa wa Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliozikutanisha timu za Simba ya Dar es salaam na Azam FC pia ya Dar es salaam.
Mashabiki wa timu ya Simba wakifuatilia mchezo huo wakati ulipokuwa ukiendelea kwenye uwanja wa Uhuru.
Mchezaji wa Simba Laudit Mavugo akiwatoka mabeki wa timu ya Azam FC Shomari Kapombe na mbele na David Mwantika katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliochezwa Jumamosi septemba 17, 2016 kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Mchezaji wa Simba Laudit Mavugo akiondoka na mpira mbele ya  mabeki wa timu ya Azam FC Shomari Kapombe kulia na  David Mwantika kushoto  katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliochezwa leo kwenye uwanja wa Uhuru
Piga nipige ikiendelea wakati wa mchezo huo.

Post a Comment

0 Comments