Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji Thobias Andengenye kulia akiongea na Mkurugenzi wa Clouds Media Ruge
Mutahaba alipotembelea ofisi za Clouds Media jana jioni, Mkurugenzi aliahidi
kutatua changamoto ya utoaji wa elimu kwa umma ya kinga na tahadhari ya majanga
ya moto inayolikabili Jeshi hilo.
(PICHA ZOTE NA FC GODFREY PETER)
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji Thobias Andengenye katikati akipata maelezo ya jinsi wanavyoendesha
kipindi cha Jahazi kutoka kwa Mtangazaji Ephraim Kibonde alipotembelea studio
za Clouds FM jana jioni 19/10/2016.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji Thobias Andengenye watatu kutoka kushoto, akiwa kwenye picha ya pamoja
na Mkurugenzi wa Clouds Media bwana Ruge Mutahaba na Watangazaji wa kipindi cha
Jahazi alipotembelea ofisi za Clouds Media jana jioni tarehe 19/10/2016.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji Thobias Andengenye akiagana na Afisa Mahusiano wa Clouds Media bwana
Simon Semalenga kwenye kuhitimisha ziara yake.




0 Comments