Random Posts

OMOG:TUMEKUJA SHINYANGA KUCHUKUA POINTI 6,LENGO LA WANA SIMBA NIKUCHUKUA UBINGWA WA LIGI MSIMU HUU.


Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
............................................
Timu ya Simba sc tayari imeshatua mkoani Shinyanga kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Mwadui FC unaotarajiwa kuchezwa mwisho mwa wiki hii huku Kocha Mkuu Joseph Omog ametamba kuwa wamekuja kuchukua alama tatu muhimu.
Akizungumza baada ya kutua Shinyanga Omog,amesema kuwa nia yetu ni kuendelea kupata matokeo mazuri kwa kila mechi tunayokutana nayo na sio kwamba tunadharau wapinzani ila msimu huu tumejiandaa kutwaa ubingwa mapema na hiyo ndio kiu ya wanasimba.
"Tumekuja kupamba na kuondoka na alama zote kwa sababu tuna mechi mbili dhidi ya Mwadui FC na Stand United hivyo hatukuja kula kutalii na tunajua michezo yote itakuwa migumu kwetu ila wachezaji wangu wapo kwa ajili ya kupata ushindi"alisema Omog
Kwa sasa Simba ndio timu pekee ambayo imecheza mechi kumi na moja bila kupoteza hata mchezo mmoja na kujikusanyia alama 29 na kuwa kinara wa Ligi huku wachezaji wakiwa na morali na kiu ya kuchukua ubingwa msimu huu na wanaonekana kuwa na uchu wa mafanikio.
Ukiangalia kila idara msimu huu imekamilika na mchezaji yoyote anayeingia anaenda kufanya kazi yake ipasavyo na kumekuwa na wafugaji wengi pindi wanapopata nafasi ya kutupia na sasa kinara ni Shiza Kichuya na Mzamiru Yassin naye ameibuka ghafla na kila mechi anacheka na nyavu tu.

Post a Comment

0 Comments