Random Posts

TFF YADAI KUWA HAIJAPATA BARUA TOKA SERIKALINI KUHUSU KUSITISHWA MFUMO WA MABADILIKO YA SIMBA NA YANGA.

Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
................................
Shirikisho la mpira wa miguu hapa nchini TFF,limesema kuwa bado hawajapokea baraua kutoka katika baraza la michezo la taifa BMT kuhusiana na taarifa yake ya usitishwaji wa mfumo wa mabadiliko yanayotakiwa kufanywa na vilabu vya Simba na Yanga.

Afsa Habari wa TFF,Alfred Lucas, amesema kuwa ingawa bado hawajapokea barua hiyo kwa ajili ya kuziwasilisha kwa vilabu husika lakini kama wao wasimamizi wa mpira wa miguu wanaendelea kuheshimu maamuzi hayo ya serikali.

Juma lililopita katibu mkuu wa BMT Mohamed Kiganja alisema kwamba baraza hilo limestisha mfumo wa hisa na ukodishwaji kwa vila vya Simba na Yanga kwa kuwa vilabu hivyo havijafuata taratibu za katiba zao,hivyo wanatakiwa kusitisha hadi hapo watakapoanza kufuata taratibu za sheria na katiba zao.

Hatua ya Serikali kusitishwa kwa mchakato huu ni kuwa kuna malalamiko mengi yanatolewa na baadhi ya wanachama kutokubaliana na jambo hilo huku wengine wakikimbilia mahakamani kupiga mchakato mzima unaohusiana na mabadiliko yanayotakiwa na vilabu vya Simba na Yanga.

Post a Comment

0 Comments