Katika harakati
za kuwania nafasi ya kufuzu kombe la Dunia nchini Urusi Mwaka 2018,timu
ya Uingereza imewachakaza mahasimu wao Scotland kwa idadi ya magoli
3-0.
Daniel
Sturridge alikuwa wa kwanza kuwanyanyua mashabaki wa Uingereza katika
dakika ya 23 akifunga goli la utangulizi akipokea mpira toka kwa Kelly
Walkers baada ya kuingia kwa goli hilo Scotland walicharuka na kuendelea
kulisakama lango la wenyeji hadi mapumziko wenyeji walikuwa mbele.
Kipindi
cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ili ziweze kuibuka
na ushindi mnamo dakika ya 50 kiungo mshambuliaji wa Liverpool Adam
Lallana alifunga goli la pili huku akipokea pasi ya Daniel Rose na
kuwafanya Scotland kuendelea kuwa wanyonge.
Gary
Cahill alipeleka msumari wa mwisho dakika ya 63 kwa kichwa mpira
uliopigwa na Nahodha Wayne Rooney na kuweza kuwapa pointi tatu muhimu na
kujiweka nafasi nzuri ya kufuzu hadi mpira unamalizika Uingereza
wameibuka na ushindi wa magoli 3-0.
Kwa
matokeo hayo vijana wa kocha Gareth Southgate wafikishe pointi 10 na
kukaa kileleni wakiwa wamecheza mechi nne kushinda tatu na sare moja.
VIKOSI:ENGLAND(4-2-3-1):Hart, Rose, Stones, Cahill, Walker, Dier, Henderson,Lallana, Rooney, Sterling, Sturridge, (Vardy.
Subs not used: Heaton, Clyne, Walcott, Jagielka, Bertrand, Townsend, Kane, Rashford, Wilshere, Lingard, Pickford
Booked: Cahill, Rooney
Goals: Sturridge 24, Lallana 50, Cahill 61
SCOTLAND (4-2-3-1):
Gordon, Anya, (Paterson ), Wallace, Hanley, Berra , Morrison
(McArthur), Brown, Darren Fletcher , Forrest , Snodgrass (Ritchie ),
Griffiths.
Subs not used: Marshall, Chris Martin, Russell Martin, Naismith, Steven Fletcher, Bannan, Burke, Kingsley, Hamilton
Booked: Griffiths
Referee: Cuneyt Cakir (Turkey) 6.5
Attendance: 87, 258
Player ratings by Sami Mokbel
|
0 Comments