Random Posts

PRISONS YASHINDWA KUFUTA UTEJA WA KUFUNGWA NA YANGA,YALALA UWANJA WA SOKOINE MECHI YA LIGI KUU TANZANIA.

Na.Alex Mthias.

Baada ya kupokea kichapo cha magoli 2-1 dhidi ya Mbeya City hatimaye mabingwa watetezi Yanga wameibuka na pointi tatu muhimu baada ya kuwasambaratisha wenyeji Tanzania Prisons goli 1-0 mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara kwenye uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Mchezo wa Leo ulikuwa mpira mkali kwa pande zote mbili huku timu zote zikitumia mchezo wa kasi muda wote huku kosakosa ziliendelea kutawala kutokana na ulinzi kuwa mzuri hadi mapumziko zilienda kupumzika zikiwa hazijafungana
Kipindi cha pili kilianza kwa Yanga kufanya mabadiliko kwa kumtoa kinda Yussuf Mhilu ambaye alianza na nafasi yake kuchukuliwa na mchezaji bora wa mwezi wa Oktoba Simon Msuva na katika dakika 54 Tanzania Prisons walikosa penati iliyopigwa na Lambert Sabiyanka kuokolewa na kipa wa Zamani wa Prisons,Benno Kakolanya  baada ya Deus Kaseke kumchezea rafu Victoria Hangaya ndani ya kumi na nane.

Dakika ya 74 Simon Msuva aliwanyanyuwa mashabiki wa Yanga ambao walifurika uwanja wa Sokoine kuisapoti timu yao akiifungia timu yake kwa njia ya mkwaju wa penati baada ya Obrey Chirwa kuchezewa rafu na beki wa Prisons James Mwasote hilo likiwa goli la sita kwa Msuva msimu huu.

Kwa matokeo hayo Yanga imefikisha pointi zao 30 katika nafasi ya pili wakiwa wanazidiwa pointi tano na watani wao Simba ambao wameonja uchungu wa kufungwa goli moja kwa bila na African Lyon na mchezo wa kufunga mzunguko wa kwanza utamaliza siku ya Jumatano itakapovaana na Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.


Kikosi cha Prisons:

Andrew Ntala, Benjamin Asukile, Salum Kimenya, Leonsi Mutalemwa, James Mwasote, Nurdin Chona, Jumanne Elfadhil, Lambarti Sabiyanka, Mohemmed Samata, Victor Hangaya/ Meshack Selemani dk82 na Jeremiah Juma/Salum Bosco dk27
Kikosi cha ⁠⁠⁠⁠Yanga:

Beno Kakolanya, Mbuyu Twite, Mwinyi Haji, Kelvin Yondan, Vicent Bossou, Haruna Niyonzima, Thaban Kamusoko, Yussuf Mhilu/Simon Msuva dk46, Donald Ngoma, Obrey Chirwa/Matheo Anthony dk90 na Deus Kaseke/Amissi Tambwe dk56.

Post a Comment

0 Comments