Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru
Kenyatta wakati nyimbo za Taifa zikipigwa kabla ya kuondoka nchini Kenya na
kurejea nyumbani Tanzania.
Rais
wa Kenya Uhuru Kenyatta akimsindikiza mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuelekea kwenye ndege katika uwanja wa Jomo
Kenyatta nchini Kenya.
Rais
wa Kenya Uhuru Kenyatta akizungumza na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta.
Rais
wa Kenya Uhuru Kenyatta akimpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli wakati alipowasili katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta
kabla ya kuondoka kurejea nyumbani nchini Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta mara baada ya kumaliza ziara yake nchini Kenya.
Picha na IKULU






0 Comments