Rais wa Jamhuri ya muungano wa
Tanzania John Pombe Magufuli amesema kuwa kwa kweli yeye ni mshabiki
mkubwa michezo na burudani lakini anashindwa kuhudhuria michezo kutokana
na baadhi ya mashabiki wa timu fulani kufanya vurugu na mpaka kufikia
hatua ya kung’oa viti uwanja wa Taifa.
DKT.Magufuli ameyaongea hayo Leo
Ikulu jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari
pamoja na wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali ambapo amesema kuwa
anashwangazwa natua hiyo ya kufanya uharibifu mkubwa katika uwanja wa
Taifa ambao ulijengwa kwa gharama kubwa tena ni kodi ya wananchi.
“Nasema kabisa bora nikaangalie mechi
za ndondo kuliko kwenye kushuhudia mpira wa Simba na Yanga wakati watu
wanang’oa viti ambavyo havina hata makosa na hawajui gharama ya
kuutengeneza huo uwanja”alisema Magufuli
Kwa kumbukumbu maneno ya Mh.Magufuli
yanazilenga klabu kongwe hapa nchini Tanzania Simba na Yanga ambapo
zilicheza Oktoba Mosi na mchezo kumalizika kwa sare ya kufungana goli
1-1 pamoja na kusababisha mashabiki kung’oa viti baada ya mshambuliaji
wa Yanga,Amis Tambwe kufunga goli ambalo liliaminika kuwa aliunawa mpira
kabla ya kufunga na kumtoa nje kiungo Jonas Mkunde kwa kadi nyekundu
hali iliyosababisha ghasia kwa mashabiki hao.
Aidha amesema kuwa hiyo ndio hali iliyosababisha kushindwa
kujitokeza viwanja kushuhudia mechi mbalimbali hivyo yeye anapenda
michezo toka moyoni mwake na pia amewaomba watu wenye tabia hiyo ya
kufanya vurugu uwanjani waache mara moja.
0 Comments