Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akionyesha mfano wa hati ya
safari ya kuelekea Mwanza kupitia Shirika la ndege la Tanzania (ATCL), kushoto
kwake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa.
Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akipokea maoni kutoka kwa wasafiri
wanaotumia usafiri wa anga katika uwanja wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere
(JNIA) wakati alipokagua utoaji wa huduma uwanjani hapo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akiongea na waandishi wa habari kabla ya kufanya ziara ya kikazi mkoani Mwanza kupitia Shirika la ndege la Tanzania (ATCL), leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akipokea maoni kutoka kwa wasafiri
wanaotumia usafiri waa anga katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere wakati
alipotembelea kukagua huduma zitolewazo uwanjani hapo.
Mkurugenzi Mtendaji wa
Shirika la ndege Tanzania (ATCL) Eng. Ladislaus Matindi akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa wakati alipotembelea Uwanja wa Kimataifa wa
Mwl. Julius Nyerere (JNIA) kukagua huduma zitolewazo uwanjani hapo.
................................................................................................
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muunngano wa Tanzania Bi Samia Suluhu amewasihi viongozi wa serikali na wananchi kutumia ndege za Shirika la Ndege
Tanzania(ATC) ili kudumisha uzalendo na kuchangia pato la shirika hilo kwa
lengo la kuhimili ushindani na kukuza uchumi wa nchi.
Ametoa rai hiyo jijini
Dar es salaam alipopewa hati ya kusafiria kupitia ndege za shirika hilo wakati
akisafiri na ujumbe wake kuelekea mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi.
“Napenda kutoa wito
kwa viongozi wa Serikali na wananchi kwa ujumla kutumia ndege zetu ili shirika
letu lifanye kazi vizuri zaidi, kufanya hivi kutaongeza pato na kukuza uchumi wa
nchi ”, amesema Makamu wa Rais.
Ametanabaisha kuwa kwa
kutumia ndege za Shirika la ATC kwa safari za ndani Serikali itaokoa fedha
nyingi zinazotumika kwa kukodi ndege za mashirika binafsi.
“Mimi na ujumbe tumeamua
kusafiri na ndege za shirika la ndege Tanzania kutokana na kubana matumizi,
gharama tuliyotumia kwa safari hii ni
shilingi Milioni saba na laki sita
ambapo tungekodi ndege binafsi tungetumia milioni arobaini”, amefafanua Makamu
wa Rais.
Kwa upande wake Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amempongeza Makamu
huyo kwa kitendo cha uzalendo alichokionyesha na kutaka viongozi wengine wa
Serikali na wananchi kwa ujumla kuiga mfano huo ili kuliinua shirika hilo na
kuongeza uchumi.
“Nampongeza Makamu wa
Rais kwa kuamua kutumia ndege za Shirika hili kwa safari za ndani, kitendo hiki
kimeonesha nia ya dhati ya serikali ya kulifufua shirika hili, naomba wananchi
nao waendelee kutumia ndege za shirika hili katika safari zao za ndani kama
alivyofanya Makamu wa Rais”, amesema Waziri Mbarawa.
Naye Mkurugenzi
Mtendaji wa Shirika hilo Mhandishi Ladislaus Matindi ameahidi kuboresha huduma
katika shirika hilo ikiwemo mifumo ya kukatisha tiketi ili kurahisisha utoaji
wa huduma na kuvutia wateja wengi kwa lengo la kurudisha hadhi ya shirika.
“Tumeshaanza mchakato
wa kuweka mfumo mpya wa kukatisha tiketi
ikiwemo kwa njia ya kielektroniki kupitia tovuti ya shirika hili ambapo mteja
hatalazimika kufika kwenye ofisi zetu”, amesema Mhandis Matindi.
Imetolewa
na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano.






0 Comments