Decemba 23, 2016.
Katika
kusheherekea msimu huu wa krismasi Multichoice Tanzania Kupitia
King’amuzi chake maarufu cha DStv imemwaga zawadi ya ving’amuzi vya
kisasa vipatavyo 24 pamoja na vifurushi vya mwezi mzima kwa
washindi wa shindano la ‘Kapu la Sikukuu’ lililoendeshwa kwa ushirikiano na kituo cha redio cha EFM.
Washindi hao
sasa wataweza kusherehekea kwa mbwembwe sikukuu ya krismass na mwaka
mpya huku wakiangalia chaneli zaidi ya 70 za DStv ikiwemo mpira wa ligi
ya Hispania (laLiga) na ligi ya Uingereza.
Pia katika kifurushi hicho wanachopata kama zawadi kina chaneli ya
Maisha Magic Bongo yenye simema na tamthilia za kitanzania ikiwemo
Tamthilia maarufu ya HUBA ambapo wakongwe wa filamu nchini kama Muhogo
Mchungu, Riyama Ali, Mboto na Hashim Kambi wanaonekana
kwenye tamthilia hiyo iliyojitwalia umaarufu mkubwa.
Katika
kunogesha hafla hiyo, Waigizaji maarufu nchini “Mboto” na “Irene Paul”
ndiyo waliokabidhi zawadi kwa washindi katika hafla hiyo iliyofanyika
jijini Dar es Salaam mapema jana.
Akizungumza
muda mfupi kabla ya washindi hao kukabidhiwa zawadi zao, Meneja Masoko
wa Multichoice Tanzania Alpha Mria alisema kampuni yao imeamua
kuwatunuku washindi hao ving’amuzi na vifurushi
vya mwezi mzima vya DStv ili kuwafanya wao na familia zao kusherehekea
krismass na mwaka mpya kwa mbwembwe na bashasha majumbani kwao huku
wakitazama DStv.
Amesema
kuwa Multichoice Tanzania hawajawatunuku washindi wa Kapu la sikukuu
tu, bali watanzania wote kwani hivi karibuni walishusha bei za
virfurushi vyao kwa wastani wa asilimia 16, huku
kifurushi maarufu cha DStv Bomba chenye chaneli zaidi ya 70
kikipunguzwa bei hadi Shilingi 19,975 tu!
Kwa mawasiliano zaidi:
Instagram (@DStvTanzania),
Twitter (@DStv_TZ), Facebook (@DStvTanzania) and website (www.dstv.com)




0 Comments