Random Posts

SHIRIKA LA NDEGE LA UTURUKI LAANZISHA SAFARI ZA ZANZIBAR




Shirika la Ndege la Uturuki limeiongeza Zanzibar katika mtandao wa safari zake kuanzia Desemba 13, 2016. Hivi sasa shirika hilo linafanya safari 49 barani Afrika baada ya hivi karibuni kuongeza safari ya kwenda Visiwa vya Shelisheli.

Shirika hilo maarufu barani Ulaya kwa sasa linafanya jumla ya safari 293 duniani kote, zikiwemo safari 50 kwenye nchi 31 za Afrika.

Likiwa ni shirika la nne kwa kuwa na mtandao mkubwa wa safari duniani kote kuliko mashirika mengine, Shirika la Ndege la Uturuki sasa litahudumia miji ya kimataifa 244 ikijumlishwa na Visiwa vya Zanzibar ambavyo ni maarufu kwa biashara ya viungo. 

Watumiaji wa ndege za shirika hilo sasa watafurahia uzoefu watakaoupata kutokana na safari hizo mpya zinazojumuisha miji 20 maarufu duniani kama vile Frankfurt, Muscat, Munchen, Dubai, Paris, London, Milano, Amsterdam, Zurich, Bombay, Copenhagen, Stockholm, Rome, Brussels, Berlin, Vienna, Hamburg, Tel-Aviv, Düsseldorf, na Prague.

Safari ya kwanza itazinduliwa Jumanne, Desemba 13, 2016 na wasafiri wataondoka Istanbul saa 6:30 usiku na ndege TK567 itakayowasili saa 3:30 asubuhi. Watarudi na ndege hiyo TK567 itakayoondoka Zanzibar saa 4:25 asubuhi na kuwasili Istanbul saa 11:45 jioni.

Safari za Instanbul – Kilimanjaro – Zanzibar – Istanbul (IST-JRO-ZNZ-IST) zitakuwa tatu kwa wiki. Utaratibu wa kuweka mpango  wa safari unapatikana kupitia tovuti www.turkishairlines.com kama ifuatavyo::
Taarifa zaidi kuhusu ratiba ya safari:

 Muda uliotajwa ni wa LMT.

Kuangalia ratiba ya safari tafadhali tazama tovuti www.turkishairlines.com, wasiliana na kituo  +90 212 444 0849 au tembelea ofisi ya mauzo ya Shirika la Ndege la Uturuki 

 Shirika la Ndege la Uturuki, Inc.
Idara ya Uhusiano


Kuhusu Shirika la Ndege la Uturuki:

Lilianzishwa 1933 likiwa na ndege tano, na ni mwanachama wa Star Alliance. Kwa sasa shirika hili lenye hadhi ya nyota nne, lina ndege 335 (za abiria na mizigo) zinazosafiri kwenye miji 292 duniani kote na kufanya safari za ndani 243 kwenye miji 49. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Skytrax wa 2016, Shirika la Ndege la Uturuki lilichaguliwa "Shirika Bora la Ulaya" kwa mara ya sita na "Shirika Bora kwa Ulaya ya Kusini  kwa mara ya nane mfululizo. Baada ya kupata tuzo mwaka 2010 ya "Shirika Bora kwa Huduma ya Chakula”, na mwaka 2013 na 2014 kuwa  "Shirika Bora kwa Biashara ya Chakula", na "Shirika Bora kwa Biashara ya Chakula kwa Wasafiri wa Daraja la Wafanyabiashara”, na tuzo ya "Shirika Bora kwa Ukumbi wa Mapumziko" hapo mwaka jana,  Shirika la Ndege la Uturuki lilipewa tena tuzo ya  “Shirika Bora kwa kuwa na “Ukumbi wa Kisasa wa Chakula” na  “Shirika Bora kwa Huduma za Chakula kwa Wasafiri” kutokana na utafiti uliofanywa mwaka huu. Taarifa zaidi kuhusu Shirika la Ndege la Uturuki zinapatikakana kwenye tovuti yake www.turkishairlines.com au kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Facebook, Twitter, YouTube, LinkedIn, and Instagram
Kuhusu Star Alliance:
Mtandao wa Star Alliance ulianzishwa 1997 ukiwa ni mtandao shirikishi wa mashirika ya ndege duniani ili kutoa huduma kwa wasafiri wa kimataifa. Kukubalika kwake kwenye soko kumetambuliwa kwa tuzo mbalimbali za Business  Traveller Magazine na Skytrax zikiwemo Tuzo ya Dunia ya Uongozi wa Soko la Usafiri wa Anga (Air Transport World Market Leadership Award) na Shirika Bora Shirikishi la Mashirika ya Ndege (Best Airline Alliance). Mashirika wanachama ni: Adria Airways, Aegean Airlines, Air Canada, Air China, Air India, Air New Zealand, ANA, Asiana Airlines, Austrian, Avianca, Avianca Brazil, Brussels Airlines, Copa Airlines, Croatia Airlines, EGYPTAIR, Ethiopian Airlines, EVA Air, LOT Polish Airlines, Lufthansa, Scandinavian Airlines, Shenzhen Airlines, Singapore Airlines, South African Airways, SWISS, TAP Portugal, Turkish Airlines, THAI and United. Kwa ujumla, mtandao wa Star Alliance sasa unasimamia zaidi safari za kila siku 18,500 kwenye viwanja vya ndege 1,330  katika nchi 192.

Post a Comment

0 Comments