Wafanyakazi
wa Tbl Group wakifurahia ushindi wa mshindi wa jumla wa Tuzo ya Mwajiri Bora
2016
Mkurugenzi wa ATE,Dk.Aggrey Mlimuka,akimpongeza Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa TBL kwa ushindi
Wafanyakazi
wa Tbl Group wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kuibuka washindi wa
jumla wa tuzo ya mwajiri Bora 2016
.....................................................................................
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imeibuka kuwa
mshindi wa jumla wa tuzo ya mwajiri bora mwaka 2016 inayotolewa na Chama Cha
Waajiri Tanzania (ATE).Ushindi huu imeupata kwa mara ya pili tena ambapo pia
mwaka jana ilikuwa mshindi wa tuzo hii ambayo inatambua taasisi inayotekeleza
vigezo vya Raslimali Watu kwa viwango vinavyotakiwa.
Hivi karibuni pia TBL ilishinda tuzo ya
mwajiri bora ngazi ya kimataifa kutoka taasisi ya kimataifa ya The Top
Employers’ Institute yenye makao yake makuu nchini Uholanzi ambayo inaanda tuzo
bora kwa makampuni yanayotekeleza vigezo vya Raslimali Watu kwa viwango vya juu
duniani.
Mbali na
kushinda tuzo kubwa za uajiri bora ,TBL pia mwaka huu inashikilia ushindi wa
jumla wa tuzo ya Rais ya Mzalishaji bora wa mwaka 2015 (President’s
Manufacturer of the Year Award (PMAYA).
Mgeni Rasmi
katika hafla ya utoaji wa tuzo hizi kwa
makampuni katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Julius Nyerere
International Convention Centre alikuwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania,Mh.Kassim Majaliwa Kassim ambaye alisema kuwa serikali
itashirikiana na sekta binafsi kwa kuzijengea mazingira bora ya kufanya biashara ili ziweze kukuza wigo wa
ajira kwa wananchi hususani vijana wenye taaluma mbalimbali wanaohitimu masomo
yao ya elimu ya juu.
Akiongelea
ushindi huo,Mkurugenzi Raslimali Watu wa TBL Group,David Magese amesema kuwa
kampuni inao wafanyakazi wapatao 2,100
wakiwemo wafanyakazi wenye ajira za muda katika biashara zake nchini
wakiwa wameajiriwa kwenye vitengo
mbalimbali vikiwemo vitengo vya ufundi,Masoko na Usambazaji.
Alisema
katika kuhakikisha wafanyakazi wanafanya kazi kwa kujituma kampuni inao
utaratibu wa kutoa MOTISHA kwa wafanyakazi wake kwa kuthamini mchango wao
katika kazi mpango ambao umefanikiwa kuongeza ufanisi na mafanikio makubwa kwa kampuni.
Mbali na
kuwapa motisha wafanyakazi wake,Magesse alisema TBL inatekeleza programu mbalimbali zenye manufaa
kwa wafanyakazi wanapokuwa sehemu za
kazi na nje ya kazi mojawapo ikiwa ni The
TBL Women’s Forum ambayo imelenga kuwajengea uwezo wafanyakazi wanawake
kutekeleza majukumu yao kwa kujiamini na kushika nafasi za uongozi kwenye
kampuni.
“Tunaendelea
kuwekeza kwa kutoa mafunzo ya kila aina ya ndani kwa ajili ya kuwanoa
wafanyakazi wetu wazidi kupata maarifa zaidi na kwendana na mabadiliko ya
teknolojia.Vile vile tunao mpango wa AFYA KWANZA ambao unahusu kuwapatia
wafanyakazi wetu na familia zao elimu ya afya na tangu uanze umeonyesha
mafanikio makubwa na wanaendelea kuufurahia.
Alimalizia
kwa kusema kuwa tuzo hizi ambazo kampuni imekuwa ikishinda katika Nyanja
mbalimbali kutoka taasisi kubwa zinazoheshimika zinazidi kuwatia moyo
wafanyakazi wote wa kampuni ambao mchango wa kila mmoja ndio unawezesha
kupatikana kwa mafanikio haya.



0 Comments