Random Posts

WANAMITINDO LEO, KUSHIRIKI NA KUSHEREKEA BIRTHDAY KWENYE SANAA FASHION SHOW

Hii ni taarifa njema kutoka kwa wanamitindo wa hapa Tanzania siku ya leo inategemea kuwa siku ya kipekee na yakuvutia pale Village Museum ambapo kutafanyika “Sanaa Fashion Show” itakayo wakutanisha wanamitindo mbalimbali. 

Kumbuka Mama wa Mitindo Maarufu kama Asya Idarous Khamsin amezaliwa tarehe kama ya leo yaani leo ni Birthday yake. Hivyo Designer mbalimbali wamejipanga kushiriki na kusherekea Sanaa Fashion Show + Birthday Party.

Shangwe nderemo na vifijo vitatawala ndani ya “Village Museum” Hongera sana Mama Asya Idarous Khamsin tunaamini wewe ni mwana mitindo mkubwa sana hapa Tanzania umeendelea kutoa hamasa na msukumu mkubwa kwa up coming designers na hatmaye baadhi yao kufikia malengo kupitia mgongo wako. Mungu akutunze,akubariki pia akuzidishie neema uzidi kuwa mfano kwa jamii inayo kuzunguka Happy to you.

Post a Comment

0 Comments