Random Posts

MA RC, DC WA AGIZWA KUHAKIKISHA WANACHUKUA HATUA DHIDI YA TATIZO LA WATOTO WAISHIO KATIKA MAZINGIRA HATARISHI NCHI.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene akizindua kitabu cha Mwongozo wa Taifa wa Utekelezaji wa Sera za Huduma kwa watoto waliokatika mazingira hatarishi kwa Serikali za Mitaa leo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Misaada na Maendeleo la Marekani (USAID)  nchini Tanzania Tim Donnay, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Theresia Mmbando, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI Dkt. Zainab Chaula na Msaidizi wa Waziri wa Nchi TAMISEMI Bi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Theresia Mmbando  akimkabidhi Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam   kitabu cha Mwongozo wa Taifa wa Utekelezaji wa Sera za Huduma kwa Watoto waliokatika mazingira hatarishi kwa Serikali za Mitaa leo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI Dkt. Zainab Chaula (wapili kulia).
 Baadhi ya washiriki wa mkutano baina ya USAID na TAMISEMI uliofanyika katika ofisi za TAMISEMI jijini Dar es Salaam wakifuatilia hoja kutoka kwa wasilishaji wa mada leo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Sekta kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dkt. Andrew Komba akichangia mada wakati wa mkutano baina ya TAMISEMI na USAID kuhusu Afya ya mama na motto leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Misaada na Maendeleo la Marekani (USAID) nchini Tanzania Tim Donnay mara baada ya kumaliza mkutano kuhusu Afya ya Mama na Mtoto leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja washiriki wa  mkutano baina ya TAMISEMI na USAID kuhusu Afya ya mama na mtoto leo jijini Dar es Salaam.Kutoka Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki, Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Misaada na Maendeleo la Marekani (USAID)  nchini Tanzania Tim Donnay,  Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI Dkt. Zainab Chaula na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Theresia Mmbando. 

Picha zote na: Frank Shija – MAELEZO.
.................................................................
Na: Frank Shija – MAELEZO
26/01/2017
WAKUU wa Mikoa na Wilaya nchini wametakiwa kuhakikisha wanatafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.
Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene wakati akizungumza na wanaandshi wa habari baada ya kumaliza mkutano wa pili wa majadiliano baina ya TAMISEMI na Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID) pamoja na uzinduzi wa Muongozo wa Taifa wa Utekelezaji wa Sera za Huduma kwa watoto waliokatika mazingira hatarishi leo jijini Dar es Salaam.
“Sera ya ugatuaji wa madaraka inaipa mamlaka Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhakikisha watoto wanaishi katika mazingira salama, natoa wito kwa Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya nchini kutimiza wajibu wao kwa kushugulikia changamoto za watoto wa mitaani,” alisema Simbachawene.
Simbachawene aliongeza kuwa Serikali za Mitaa zinao wajibu wa kuwahudumia watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwa ndiyo watekelezaji wa sera mbalimbali ikiwemo sera ya watoto, viongozi wa Serikali za Mitaa wasiishie tu kuwaondoa watoto mitaani bila ya kutafuta kiini na suluhisho la tatizo hilo.
Aidha Simbachawene amempongeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kazi nzuri ya utafiti ambayo imebaini kuwa rasilimali nyingi zinazotengwa kwa ajili ya kuhudumia afya ya mama na motto haziwafikii walengwa ambapo amesema kuwa hiyo ni changamoto kubwa.
Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Magufuli inasisitiza uwazi na uwajibikaji hivyo panapotea kuwa uzembe unatokana na utendaji mbovu miongoni mwetu si vyema tukafumbia macho badala yake inapaswa tuseme ukweli ili wahusika wajirekebishe na kuchukuliwa hatua stahiki.

Post a Comment

0 Comments