MASHIDANO YA VIKUNDI VYA MAZOEZI KUANZA RASMI NCHINI. - MTAZAMO MEDIA

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, 14 January 2017

MASHIDANO YA VIKUNDI VYA MAZOEZI KUANZA RASMI NCHINI.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bw. Felix Lyaniva wa pili kulia wakiongoza mazoezi wakati wa uzinduzi wa mazoezi katika mkoa huo uliofanyika wilaya ya Temeke yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bw. Felix Lyaniva anayemfuatia kulia wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanamazoezi wakati wa uzinduzi wa mazoezi mkoa huo katika wilaya ya Temeke yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
 Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bw. Felix Lyaniva kushoto akiongea na wanamazoezi wa mkoa wa Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa mazoezi mkoa huo katika wilaya ya Temeke yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.
NA Ally Daud-WIZARA YA AFYA.

MASHINDANO ya vikundi vya kufanya mazoezi yanatarajiwa kuanza hivi karibuni jijini Dar es salaam na mikoa mingine ili kutekeleza kauli na agizo la Mhe. Makamu wa Rais wa Awamu ya Tano Bi. Samia Suluhu Hassan alilolitoa wakati anazindua kampeni ya kitaifa ya kufanya maoezi Desemba 17 2016.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa ufunguzi wa mazoezi ya hiari mkoa wa Dar es salaam yaliyofanyika katika wilaya ya Temeke.

“Hata kama zawadi ikiwa ng’ombe lazima kipatiane kikundi kimoja cha mazoezi ambacho ni bora kuliko vikundi vingine mkoa mpaka kitaifa ili kuwafanya watanzania waepuke magonjwa yasioambukiza kwa kupenda mazoezi.

Aidha Mhe. Ummy amesema kuwa kampeni hiyo ya kufanya mazoezi inalenga zaidi kupunguza gharama za kutibu ugonjwa huo na badala yake kuwataka watazania kufany mazoezi siku tatu katika wiki ngalau kwa dakika 30 il kujikinga na magonjwa yasiomabukiza.

Kwa upande wake Mkuu Wa wilaya ya Temeke Bw. Felix Lyaniva amesema kuwa mazoezi hayo yamewahamasisha na wamepanga kila ijumaa wafanyakazi wote wa umma wanatakiwa kufanya mazoezi ili kujikinga na magonjwa yasioambukiza.

Aidha Bw. Lyaniva amesema kuwa wtanzania wanapaswa kufanya mazoezi ili kuweza kujipunguzia gharama za matibabu ya magonjwa yasioambukiza ili kujenga taifa lenye wananchi wenye afya imara.

Kampeni hiyo ya kufanya mazoezi ya kitaifa  ina lengo la kujikinginga na magonjwa yasioambukiza kam vile kisukari, magonjwa ya moyo, saratani, shinikizo la damu na magonjwa ya mfumo wa hewa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages