Random Posts

RAIS WA UTURUKI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI

 Rais wa  Uturuki,  Mheshimiwa  , Recep Tayyip Erdogan akiongozana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam kwa ziara rasmi Januari 22, 2017.Mheshimiwa Majaliwa alimpokea Rais huyo kwa niaba ya Rais John Magufuli.

 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa   na Rais wa Uturuki, Mheshimiwa Recep Tayyip Erdogan  aliyefuatana na  mkewe, Mheshimiwa Emine Erdogan (kulia) wakifurahia ngoma kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage jijini Dar es salaam baada ya Rais huyo  kuwasili kwa ziara rasmi nchini Januari 22, 2017. Mheshimiwa Majaliwa alimpokea Rais huyo kwa niaba ya Rais John Magufuli.

 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Rais wa Uturuki, Mheshimiwa Recep Tayyip Erdogan akiagana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa baada ya kumfikisha kwenye hoteli ya Serena  jijini Dar es salaam  baada ya kumpokea kwenye uwanja wa ndege wa Dar es salaam na kumsindikiza hadi kwenye hoteli hiyo alikofikia Januari 22, 2017.

 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
...................................................................
                    
RAIS wa Uturuki Mheshimiwa Recep Erdogan amewasili nchini leo jioni (Jumapili, Januari 22, 2017) kwa ziara ya kikazi ya siku mbili na kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupokelewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na niaba ya Mheshimiwa Rais. Dkt. John Magufuli.
Rais huyo ameambatana na mkewe Mama Emine Erdogan pamoja na Mawaziri watatu ambao ni Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Mevlüt ÇavuÅŸoÄŸlu, Waziri wa Uchumi Mheshimiwa Nihat  Zeybekekci na Waziri wa Nishati na Maliasili Mheshimiwa Berat Albayrak
.
Pia Rais huyo ameambatana na wafanyabiashara wapatao 85 wa nchi hiyo.
                            
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 - DAR ES SALAAM

JUMAPILI, JANUARI 22, 2016.

Post a Comment

0 Comments