Random Posts

JAFO AWATAKA WANAFUNZI NA WALIMU SHULE YA CHANG'OMBE MANISPAA YA DODOMA KUTUNZA MIUNDOMBINU YA SHULE ILI KUONGEZA UFAULU

 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Seleman S.Jafo akizungumza na walimu, wanafunzi na Kamati ya shule ya msingi Chang’ombe A Manispaa ya Dodoma alipofanya ziara kujionea maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa ambao umekamilka kwa asilimia mia moja. Kulia kwake ni Kaimu Afisa Elimu Mkoa Dodoma Bw. Tumsifu Mwasamale na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bi. Nelly kinyaga kushoto kwake ni Diwani Kata ya Chang’ombe Mhe.Bakari Samweli Fundikira
 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Seleman S.Jafo akifungua mlango ili kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa ambao umekamilika kwa asilimia mia moja

 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Seleman S. Jafo akitoa agizo kwa halmashauri, kamati za shule na mikoa nchini kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kutumia juhudi na maarifa ili kuwaletea wananchi maendeleo kwa haraka. Ameridhishwa na ubora na kasi waliyoitumia kujenga majengo hayo
Mojawapo ya madarasa yaliyokamilika katika shule ya msingi Chang’ombe A Manispaa ya Dodoma. Jumla ya vyumba vya madarasa sita vimejengwa ili kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa katika shule hiyo inayotokana na wingi wa wanafunzi, shule hiyo ina zaidi ya wanafunzi 2000
.......................................................................

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na  Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe. Seleman Jafo ametoa pongezi  kwa  utekelezaji wa agizo alilolitoa  tarehe 03 Nov 2016 kwa  uongozi wa  Halhamashauri ya Manspaa ya Mji wa  Dodoma alipofanya ziara ndogo  katika kata hiyo na kubaini changamoto mbalimbali katika shule ya msingi ya Chang’ombe A .
Mhe. Waziri ametoa pongezi  hizo kwa uongozi wa Halmashauri ya  Manispaa , kamati ya shule ya Chang’ombe ,walimu na Diwani wa Kata ya Chang’ombe leo,  alipotembelea shule hiyo kukagua utekelezaji wa agizo  juu ya kukamilika kwa  ukarabati wa miundombinu  katika  shule hiyo  ifikapo 10 januari  ambapo ameridhishwa  kwa  hatua nzuri  ya  ukarabati huo.
‘’Maagizo niliyoyatoa yalikuwa magumu sana lakini nia yangu ilikuwa kuwatengenezea mazingira rafiki  wanafunzi na walimu   , nimefarijika na utekelezaji wake, hali haikua nzuri hapo mwanzo lakini nimefarijika kwa  kazi nzuri, muonekano wa madarasa unaridhisha  nawapongeza sana’’  aliongeza kwa kutoa pongezi kwa SUMA JKT kwa kukamilisha kazi kwa wakati na katika kiwango stahiki.  
 Pia Mhe. Suleman Jafo  amewataka wanafunzi na walimu wa shule ya msingi ya Chang’ombe  kutunza   na kuitumia  miundombinu hiyo rafiki ili kuongeza ufaulu katika shule hiyo na  kuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa shule nyingine .
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bi. Nelly  Kinyaga  ameishukuru serikali kwa kuboresha miundombinu ya shule  hiyo  ambapo awali mazingira ya shule hiyo yalikuwa sio  rafiki kwa wanafunzi na walimu  kutokana na  upungufu wa matundu 20 ya vyoo na  vyumba vya madarasa 8.
‘’ kwakweli kulikua na changamoto sana wanafunzi walikua wengi na madarasa machache  lakini kwasasa hatuna watoto wanaokaa chini na msongamano wa wanafunzi darasani umepungua kwa kiasi kikubwa  ,naishukuru serikali na Mhe. Jafo kwa kutilia mkazo  ukarabati wa miundombinu ya shule yetu’’ alisema
Ally Mohamed Swalehe mmoja wa wanafunzi wa shule ya Msingi Chang’ombe  ameishukuru serikali kwa kuboresha miundombinu ya shule hiyo rafiki  kwakuwa itaongeza ufaulu katika mitihani  na kuepusha magonjwa ya  milipuko shuleni hapo.

 Mhe. Waziri alitoa agizo hilo Tar 03  Nov alipofanya ziara ndogo ya kutembelea Kata ya Chang’ombe ambapo katika ziara hiyo  alitoa agizo kwa Halhamashauri ya Manispaa ya Dodoma kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa matundu 20 ya vyoo na vyumba vya  madarasa 8 pamoja  na ukarabati wa vyumba vya madarasa  2 katika shule ya Chan’gombe A  ifikapo tarehe 10 januari 2017 kabla ya msimu wa masomo kuanza.

Post a Comment

0 Comments