Random Posts

KLOPP AWAPA MATUMAINI MAPYA MASHABIKI WA LIVERPOOL

Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp amewapa matumaini mapya mashabiki wa timu hiyo kuwa katika michezo 14 ambayo imesalia kabla ya kumaliza msimu watashinda michezo yote hali ambayo itaiweka klabu hiyo katika nafasi nzuri kama ni kushinda ubingwa au kupata nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Liverpool kwa sasa ipo nafasi ya tano ikiwa na alama 46, alama 13 nyuma ya viongozi wa ligi Chelsea, lakini Klopp amesema katika soka kila jambo linawezekana na imani yake ni kushinda michezo yote 14 ambayo ipo mbele yao.
“Katika ndoto zangu tunaweza kushinda michezo 14, najua inaweza kupokelewa tofauti lakini siwezi kubadili ndoto zangu na hilo ndilo ninalolifanyia kazi na baada ya michezo 14 utakuwa muda wa kuangalia ni nini tumejifunza kutoka kwa wengine alafu tutafanya maamuzi ambayo yanaweza kutusaidia kwa msimu ujao,” alisema Klopp.

Ndoto ya Klopp kushinda michezo 14 itaanza kupimwa leo usiku wakati Liverpool itakapokuwa mwenyeji wa Tottenham kwenye uwanja wa Anfield, Tottenham wao wana alama 50 na wakiwa nafasi ya pili ya msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Post a Comment

0 Comments