Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akifanyiwa uchunguzi wa macho na
madaktari kutoka Shirika la Specsavers la Swiden walipofika Zanzibar kutoa
huduma hizo.
Dkt. Happness Urasa kutoka Shirika la Specsavers na Dkt. Abdulrahman Abdalla
wa Kliniki ya macho Mikunguni wakiwafanyia kipimo cha uoni wa mbali wa macho wagonjwa
waliofika Skuli ya Kiembesamaki kwa ajili ya kupatiwa miwani.
Baadhi ya wananchi waliofika Skuli ya msingi Kiembesamaki wakisubiri zamu
zao kupimwa uoni wa macho na kupatiwa miwani.
Daktari wa macho kutoka Shirika la
Specsavers la Swiden akiwachagulia miwani wananchi waliopatiwa huduma ya
kupimwa uoni wa macho waliofika Skuli ya msingi Kiembesamaki kupatiwa huduma
hiyo.
Picha na
Makame Mshenga-Maelezo.





0 Comments