Mchungaji
wa Kanisa la Ufunuo, Nabii Paul Bendera akiongoza ibada katika kanisa hilo leo kabla ya kumkaribisha mgeni
rasmi Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita Charles kuzumgumza na
waumini wa kanisa la ufunuo.
Mchungaji wa kanisa la Ufunuo, Nabii Paulo Bendera (kushoto) akimtambulisha mgeni rasmi kwa waumini Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita Charles kwaajili yakuzumgumza na waumini wa Kanisa la Ufunuo na kujumuika kwenye ibada ya jumapili leo.
Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita Charles akizungmza na waumini wa Kanisa la Ufunuo wakati aliposhiriki ibada ya jumapili.
Waumini wa kanisa la Ufuno wakipiga makofi kumpongeza Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita Charles wakati akizunguza.
Waumini wa Kanisa la Ufunuo wakishikishiriki kwenye ibada.
Meya
wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita (kulia) pamoja
na Mchungaji wa kanisa la Ufunuo, Nabii Paul Bendera
(katikati) wakiwa kwenye ibada ya jumapili.
Waumini wakiwa kwenye maombi ya ibada ya jumapili .
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kushiriki ibada ya jumapili kwenye kanisa la ufunuo lililoko kimara jijini Dar es Salaam.
Mchungaji
wa kanisa la Ufunuo, Nabii Paulo
bendera akifafanua jambo kwa waandishi wa habari.
.......................
Na Antony John Glob ya Jamii.
Meya wa jiji
la Dar es salaam Isaya
Mwita amewasihi wazazi
kushirikiana na serikali katika maswala
ya elimu ili kuweza kutatua tatizo la
kufeli katiaka shule za Serikali.
Kauli hiyo ameitoa leo hii wakati akifanaya aliposhiriki ibada katika Kanisa la Ufunuo linaloogozwa na Nabii Paulo Bendera, lililopo Kimara Jijini Dar es salaam amesema
wazazi wanatakiwa kuchunguza watoto wao katika masomo kwakuwa baadhi ya watoto wanaaga wanakwenda shule lakini
hawafiki hivyo inapelekea watoto kutokufanya vizuri.
''Nawasii
wazazi na walezi waendelee kushirikiana
na serikali pamoja na bodi ilikuweza kupunguza matokeo mabaya katika mkoa
wetu lakini wazazi wawakataze watoto wao kutumia simu kwa sababu watoto wengi
wanatumia simu muda mwingi kuliko muda
wa kusoma''amesema Mwita
Nae Mchungaji wa kanisa hilo la Ufunuo Nabii Bendera ameliombea Taifa amani na kuwahasa watanzania kushirikiana ili waweze kuwa na
maendeleo ya kiuchumi.
'' Nawaomba
watanzania waandelee kuitunza amani na
kuwaombea viongozi wetu kwakuwa
tusipokuwa na amani na ushirikiano hatutoweza kufikia maendeleo tunayo
yaitaji'' amesema Bendera










0 Comments