Random Posts

REA III KUJA NA UMEME MWINGI

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akiongea jambo wakati akiwaeleza wananchi na wanafunzi wa Shule ya Msingi na Sekondari ya Nyamagongo Wilaya ya Rorya kuhusu utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya III. Shule hiyo ni miongoni mwa maeneo ambayo yatafikiwa katika mradi wa REA awamu ya Tatu. Wengine wanaofuatilia ni Meneja wa TANESCO   Kanda ya Ziwa  Mhandisi Amos Maganga, (katikati) Meneja wa TANESCO  Wilaya ya Rorya, Sospeter Kswahili (wa kwanza kulia). Wengine ni Mtaalam kutoka Wakala wa Nishati Vijijini Mhandisi Emmanuel Yesaya na Mkandarasi wa Kampuni ya Angelica International.
 Afisa Uhusiano na Huduma za Jamii kwa Wateja kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),  James Vesso, akitoa elimu kuhusu Kifaa cha Umeme Tayari (UMETA) kwa wananchi wa Kijiji cha Muriaza Kata ya Muriaza Wilaya ya Butiama  wakati wa Ziara ya Waziri wa Nishati na Madini kijijini hapo. Kifaa hicho hakihitaji mtandao wa umeme katika nyumba.

 Meneja wa TANESCO   Kanda ya Ziwa  Mhandisi Amos Maganga, akizungumza jambo wakati wa mkutano wa Waziri wa Nishati na Madini wananchi wa  Nyamagongo  ambapo Waziri na wataalam wa REA na TANESCO wameeleza kuhusu utekelezaji wa REa Awamu ya Pili na ya Tatu. Wengine ni Mameneja wa TANESCO,  Wilaya ya Rorya na Mkoa wa Mara, na Wataalam kutoka REA na TANESCO.
 Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Saimon Chacha na viongozi wa Mkoa, wakimkaribisha Waziri wa Nishati na Madini  Profesa Sospeter Muhongo (kulia) wilayani humo kwa ajili ya ziara ya kukagua miradi ya REA awamu ya II na kueleza mipango ya Serikali kuhusu utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu.
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO),  Mhandisi Hamis Komba, akiwaeleza wachimbaji wadogo kuhusu shirika hilo kuridhia kutoa sehemu ya eneo lake la Buhemba kwa ajili ya wachimbaji kufanya shughuli za uchimbaji madini.
 Mtendaji Kata wa Mirwa, Neema Philipo,akisoma majina ya vikundi vya wachimbaji wadogo ambavyo vitapewa sehemu ya eneo la STAMICO, Buhemba. Wengine wanaofuatilia ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kushoto), Kaimu Mtendaji Mkuu wa STAMICO, Mhandisi Hamis Komba, (wa kwanza kushoto) Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Ziwa Viktoria Mashariki, Mhandisi Juma Sementa na Watendaji kutoka STAMICO na wachimbaji wadogo.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akitoa rambirambi kwa baadhi ya wazazi ambao mmoja wa wachimbaji wadogo alifariki katika ajali ya kifusi iliyotokea katika mgodi  eneo la Buhemba, Mkoani Mara.
 Sehemu ya wananchi wa wananfunzi katika  eneo la Nyamagongo Wilaya ya Rorya Mkoa wa Mara wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, hayupo pichani
Naibu Mhariri wa Gazeti la Jamhuri Jackton Manyerere (wa pili kulia) akiongea jambo wakati  Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akitoa heshima katika Kaburi la Baba Mzazi wa Manyerere., Jakcton Nyambereka Nyerere aliyefariki dunia tarehe 19/2/2017/. Wa kwanza kulia ni Mhariri wa gazeti la Mtanzania Kulwa Keredia. Kushoto ni baadhi ya waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari. Waziri alifika kuhani msiba wa wahariri hao Manyerere na Keredia wakati wa ziara yake Wilayani Butiama. 

Post a Comment

0 Comments