Random Posts

TIMU YA KISIJU PWANI NA TENGELEA FC ZAFANIKIWA KUCHUPA HATUA YA FAINALI MICHUANO YA ULEGA CUP 2017

1
Mchezaji  wa timu za Kisiju Pwani kulia wa kushoto akijaribu kumtoa beki wa timu ya Lukanga Fc wakati wa kivumbi cha mashindano ya ULEGA CUP hatua ya nusu fainai iliyopigwa kwenye uwanja wa shule ya msingi mkuranga,Kisiju waliibuka na ushindi wa bao 1-0 na kutinga hatua ya fainali.
2
Mchezaji wa timu ya Lukanga Fc wa kushoto akiwa katika harakati zake za kuwapita wachezaji wa timu ya Kisiju Pwani katika mchezo wa kwanza wa hatua ya nusu fainali ya michuano ya ULEGA CUP kwenye uwanja wa shule ya msingi Mkuranga.

3
Wachezaji wa timu zote mbili wakiwa uwanjani kuisakata kabumbu katika mchezo wa nusu fainali hiyo.

(PICHA NA VICTOR MASANGU)
...............................................

NA VICTOR MASANGU, MKURANGA

TIMU mbili za soka za Kisiju Pwani pamoja na Tengelea Fc zimefanikiwa kukata  tiketi ya kutinga katika hatua ya fainali baada ya kuibuka na na ushindi katika michezo miwili waliyoicheza hatua ya nusu fainali  kwenye  kinyang’anyiro cha  michuano ya ‘ULEGA CUP 2016-2017 ’ kwenye uwanja wa shule ya msingi Mkuranga mkoani Pwani.

 Michuano hiyo ambayo imeandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdalah Ulega kwa lengo la kuweza kuibua na kukuza vipaji vya wachezaji mchezo wa kambumbu ambao walishirikishwa kutoka katika kata zote 25 zilizopo katika jimbo hilo.

Katiha mchezo wa hatua ya nusu fainali ya kwanza iliweza kuzikutanisha timu ya Kisiju Pwani ambao walimenyana na majirani zao wa karibu timu ya Lukanga Fc ambapo timu ya  Kisiju ndio iliyoweza kuchupa fainali baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wapinzani wao.

Bao la washindi katika mtanange huo liliwekwa kimiani na mshambuliaji wao wa kutumainiwa Mudy Mbete kunako katika dakika ya 71 baada ya kuachia shuti kali lilizozama moja kwa moja langoni na kumwacha mlinda mlango wa timu ya Lukanga Fc  amebaki mdomo wazi.

Mchezo mwingi wa hatua ya nusu fainali ya pili ambao ulikuwa unasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa na wadau na mashabiki wa mchezo  huo timu ya ulizikutanisha timu ya Tengelea Fc ambao walicheza na Mwandege ambapo Tengelea waliibuka na ushindi wa bao 1-0 lililopachikwa na mchezaji Andrwe Joseph kunako katika dakika ya 80 na kufanikiwa kupata nafasi ya kucheza hatua ya fainali.

Kwa matokeo hayo timu ya Kisiju Pwani pamoja na timu ya Tengelea Fc ambao ndio wameweza kushinda katika michezo yao ya nusu fainali watakutana uso kwa uso katika mchezo wa fainali unaotarajiwa kufanyika machi  5  mwaka huu kwenye dimba la shule ya msingi Mkuranga.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdlah Ulega ambaye ndio mwandaaji wa mashindano hayo ya soka alisema kwamba nia yake kubwa ni kuunda timu ya Jimbo ambayo itakuwa ikishiruki katika ligi mbali mbali na ndoto yake kubwa ni kuhakikisha nashirikina na wadau wa soka ili kuwa na kikosi kizuri amabcho kitaweza kushiriki ligi kuu ya Tanzania bara katika siku za usoni.

Post a Comment

0 Comments