Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt.
John Pombe Magufuli akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya
kumwapisha Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Jenerali Venance Mabeyo na
Kamishina wa Magereza leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Jenerali
Venance Mabeyo akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)
Jenerali Venance Mabeyo akiweka saini katika hati ya kiapo cha utii mbele ya
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa
hafla ya kuapishwa kuwa Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (CDF) leo Ikulu
jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt.
John Pombe Magufuli akiweka saini katika
hati ya kiapo cha utii wakati wa hafla ya kumwapisha Mkuu wa Jeshi la Wanchi
Tanzania (JWTZ) Jenerali Venance Mabeyo leo jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt.
John Pombe Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Mkuu mpya wa Jeshi la Wananchi
Tanzania (JWTZ) Jenerali Venance Mabeyo leo
jijini Dar es Salaam.
Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Meja
Jenerali James M. Mwakibolwa akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania
Major Jenerali James M. Mwakibolwa akiweka saini katika hati ya kiapo cha utii
mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli
wakati wa hafla ya kuapishwa kuwa Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (CDF) leo
Ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John
Kijazi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt.
John Pombe Magufuli akiweka saini katika
hati ya kiapo cha utii wakati wa hafla ya kumwapisha Mnadhimu Mkuu wa Majeshi
ya Ulinzi Tanzania Meja Jenerali James M. Mwakibolwa leo jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt.
John Pombe Magufuli akimkabidhi vutendea
kazi Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Major Jenerali James M.
Mwakibolwayo wakati wa hafla ya kuwapisha
wateule hao leo jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa akila
kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe
Magufuli leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi
Balozi John Kijazi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt.
John Pombe Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Kamishna Jenerali wa Magereza Dr.
Juma Malewa wakati wa hafla ya kuwapisha wateule hao leo jijini Dar es Salaam.
Balozi Paul Mella ambaye ataiwakilisha nchi ya Tanzania nchini
katika Jamhuri ya Demokrasia ya Congo akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu jijini Dar
es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Balozi Samweli William Shelukindo ambaye
anakwenda kuiwakilisha Tanzania nchini Ufaransa akila kiapo cha utii mbele ya
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu
jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Nyakimura
Mathias Mhoji akila kiapo cha utii mbele
ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu
jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI)
Kamishna Robert Boaz Mikomangwa akila kiapo cha utii mbele ya Mkuu wa Jeshi la
Polisi Tanzania Inspekta Jenerali Ernest Mangu katika hafla ya kuwaapisha
baadhi ya viongozi walioteuliwa na Mhe. Rais kushika nyazifa mbalimbali leo
Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt.
John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi
Tanzania Jenerali Venance S. Mabeyo ( kulia) mara baada ya hafla ya kumuapisha
leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mnadhimu wa Jeshi hilo Meja Jenerali
James Mwakibolwa, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Mohamed Shein na
Waziri Mkuu wa Kassim Majali.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ)
Jenerali Venance S. Mabeyo akifurahia jambo na Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali
Davis Mwamunyage wakati wa hafla ya kuapishwa kwake leo jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na
baadhi ya Makamishna wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ya Tanzania wakati wa
hafla ya kuwaapisha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Mnadhimu Mkuu wa
Majeshi ya Ulinzi, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Mabalozi pamoja na
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma leo jijini Dar es Salaam.
............................................................
Beatrice Lyimo -
MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa vyombo vya
ulinzi kuendeleza vita dhidi ya biashara haramu ya dawa za kulevya nchini.
Rais Magufuli
ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kuwaapisha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania
Jenerali Venance Salvatory Mabeyo na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali
James Aloyce Mwakibolwa.
Rais amesema kuwa
kitendo cha Mkuu wa Jeshi la Polisi Ernest Mangu kuwasimamisha baadhi ya watendaji
kazi wake kimeipa heshima jeshi la polisi nchini.
“Madawa ya Kulevya
yanapoteza nguvu kazi za watanzania hasa vijana, hivyo hii kazi si ya mtu mmoja
ni ya wanzania wote kushirikiana kwa pamoja katika kupambana na jambo hili kwa
manufaa ya nchi” alifafanua Rais Magufuli.
Mbali na hayo alisema
kuwa, katika mapambano vipo vikwazo kadha vitakavyojitokeza hivyo watanzania
wanabudi kuungana kwa pamoja dhidi ya wafanyabiashara wa madawa ya kulevya.
Katika hatua hiyo
Rais Magufuli alisema kuwa kwa sasa nchi inavyoelekea katika uchumi wa kati
kupitia viwanda, amelitaka Jeshi la Ulinzi nchini kusimamia na kujenga nchi ya
viwanda kwa vitendo.
“haiwezekana Tanzania
ya leo bado inaagiza sare kutoka china,wakati nchi yetu ina wakulima wazuri wa
pamba, hivyo vyombo vya ulinzi mnatakiwa kujipanga katika hili, mkiamuua
kuzungumza na baadhi ya viwanda na kuwapa vipimo na ubora wa nguo, rangi
watatengeneza. ”alisema Rais Magufuli.
Alisema kuwa si kila
kitu lazima kununua kutoka nje, ni lazima kujipanga kwa kuhakikisha dhana ya
viwanda inaanzia jeshini.
“Tubadilike
tutengeneze Tanzania kwanza, maslahi ya nchi yapewe kipaumbele, rasilimali
zilizopo zitumike kwa manufaa ya nchi” alisisitiza Rais Magufuli.
Katika hatua hiyo
Rais Magufuli alitoa wito kwa majeshi nchini kutoa ushirikiano kwa wateule, kwa
kuhakikisha wanafanya kazi kwa manufaa ya nchi na askari wengine.
Kwa upande wake Rais
wa Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Ali Shein alisema kuwa jeshi la Tanzania linasifa
kubwa ndani na nje ya nchi hivyo anaamini wateule wapya watafanya kazi hiyo kwa
umahiri mkubwa.
Naye Jenerali Mstaafu
Davis Mwamunyange alisema kuwa katika kipindi cha uongozi wake, ajali ya
milipuko ya mabomu yaliyotokea Mbagala na Gongola mboto ndio kilikuwa kipindi
kigumu kwake kwani watu waliumia na mali za wananchi na za jeshi zilipotea.
Wakati huo Jenerali
Mkuu wa Majeshi aliyeapishwa leo Venance Mabeyo ameahidi kuendeleza na
kuimarisha ulinzi wa taifa la Tanzania pale ambapo Jenerali Mstaafu Mwamunyange
alipoishia na kama ilivyo majukumu ya jeshi kimsingi.
Rais Magufuli pia aliwaapisha
Kamishina Jenerali wa Magereza Dkt Juma Alli Malewa ambaye alikuwa Kamishina wa
Sheria na Uendeshaji wa Taifa la Magereza.
Wengine ni Balozi Paul
Mella ambaye ataiwakilisha nchi ya Tanzania nchini katika Jamhuri ya Demokrasia
ya Congo, Balozi Samweli William Shelukindo ambaye anakwenda kuiwakilisha
Tanzania nchini Ufaransa pamoja na Nyakimura Mathias Mhoji ambaye amekuwa
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma.
Naye Inspekta
Jenerali wa Polisi IGP Ernest Mangu amemuapisha Kamishina wa Polisi Robert Boaz
Mikomangwa ambaye amekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai.


















0 Comments