Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhandisi Hamad Masauni(kushoto), Kamanda wa Polisi Mkoa
wa Pwani (RPC), Onesmo Lyanga wakiwasili Kituo cha Polisi Bungu, Wilaya ya
Kibiti mkoani Pwani. Masauni alifanya ziara katika Kituo hicho naalizungumza na
askari Polisi wanaolinda amani katika eneo hilo na pia alizungumza na wananchi ambapo
aliwataka watoe ushirikiano kwa Jeshi hilo katika mapambano ya kuwasambaratisha
wahalifu mbalimbali waliopo Wilaya ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani humo.
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na askari Polisi wanaolinda usalama katika
Wilaya ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga ambao wameweka Kambi katika Wilaya ya
Kibiti kwa lengo la kupambana na wahalifu katika Wilaya hizo. Masauni pia
alizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Bungu na kuwahakikishia usalama
wao na pia aliwataka kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili waweze
kuwasambaratisha wahalifu hao kwa uharaka zaidi.
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia) akimsikiliza Mkazi wa Kijiji cha Bungu,
Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani, Ayubu Mketo alipokuwa anamuuliza swali
kuhusiana na hali ya usalama katika eneo lao la Bungu. Hata hivyo, Masauni aliwahakikishia
usalama wananchi wa Wilaya hiyo pamoja na ya Rufiji na Mkuranga,kuwa askari
wakewameweka kambi kwa ajili ya kupambana na wahalifu pamoja na kuwalinda
wananchi wa maeneo hayo. Masauni alifanya ziara katika maeneo hayo ambapo
alizungumza na polisi pamoja na wananchi kuhusu kushirikianana Jeshi la Polisi bila
woga ili Jeshi hilo liweze kupambana na wahalifu kikamilifu.
Picha
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhandisi Hamad Masauni(kushoto) akizungumza na mamia ya Wananchi wa Kijiji cha
Bungu, Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani. Masauni alifanya ziara katika Wilaya
hiyo kwa lengo kuangalia hali ya usalama wa Wilaya ya Rufiji, Kibiti na
Mkuranga ambapo alizungumza na askari polisi wanaolinda usalama katika maeneo
hayo na baadaye alizungumza na wananchi na kuwaomba kutoa ushirikiano kwa Jeshi
la Polisi bila woga ili waweze kuwasambaratisha wahalifu katika maeneo hayo.
Picha
zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.




0 Comments