Random Posts

MASAUNI AZUNGUMZA NAMAMIA YA WANANCHI, AWATAKA KUSHIRIKIANA NA POLISI KUWAFICHUA WAHALIFU KIBITI, MKURANGA NA RUFIJI MKOANI PWANI

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kushoto), Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani (RPC), Onesmo Lyanga wakiwasili Kituo cha Polisi Bungu, Wilaya ya Kibiti mkoani Pwani. Masauni alifanya ziara katika Kituo hicho naalizungumza na askari Polisi wanaolinda amani katika eneo hilo na pia alizungumza na wananchi ambapo aliwataka watoe ushirikiano kwa Jeshi hilo katika mapambano ya kuwasambaratisha wahalifu mbalimbali waliopo Wilaya ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani humo. 
Picha zote  na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na askari Polisi wanaolinda usalama katika Wilaya ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga ambao wameweka Kambi katika Wilaya ya Kibiti kwa lengo la kupambana na wahalifu katika Wilaya hizo. Masauni pia alizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Bungu na kuwahakikishia usalama wao na pia aliwataka kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili waweze kuwasambaratisha wahalifu hao kwa uharaka zaidi.
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia) akimsikiliza Mkazi wa Kijiji cha Bungu, Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani, Ayubu Mketo alipokuwa anamuuliza swali kuhusiana na hali ya usalama katika eneo lao la Bungu. Hata hivyo, Masauni aliwahakikishia usalama wananchi wa Wilaya hiyo pamoja na ya Rufiji na Mkuranga,kuwa askari wakewameweka kambi kwa ajili ya kupambana na wahalifu pamoja na kuwalinda wananchi wa maeneo hayo. Masauni alifanya ziara katika maeneo hayo ambapo alizungumza na polisi pamoja na wananchi kuhusu kushirikianana Jeshi la Polisi bila woga ili Jeshi hilo liweze kupambana na wahalifu kikamilifu.
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kushoto) akizungumza na mamia ya Wananchi wa Kijiji cha Bungu, Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani. Masauni alifanya ziara katika Wilaya hiyo kwa lengo kuangalia hali ya usalama wa Wilaya ya Rufiji, Kibiti na Mkuranga ambapo alizungumza na askari polisi wanaolinda usalama katika maeneo hayo na baadaye alizungumza na wananchi na kuwaomba kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi bila woga ili waweze kuwasambaratisha wahalifu katika maeneo hayo. 
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Post a Comment

0 Comments