Random Posts

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAENDELEO YA JAMII YAKAMILISHA KIKAO CHA KUPITIA BAJETI YA WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO MJINI DODOMA KABLA YA VIKAO VYA BUNGE LA BAJETI KUANZA

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy A. Mwalimu akitoa ufafanuzi wa Utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa Bajeti ya mwaka 2016/17 katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii, wakati wa mapitio ya Bajeti ya mwaka 2017/18 kwa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Kamati hiyo chini ya Uenyekiti wa Mhe. Musa Azzan Zungu (Mb, wa pili kulia) imejadili na kuridhia Taarifa ya bajeti ya Wizara hiyo siku chache kabla ya kuanza kwa vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotarajiwa kuanza mapema mwezi Aprili, 2017. Kushoto, anayefuatilia maelezo ni Naibu Waziri Mhe. Hamisi A. Kigwangalla (Mb). Kikao hicho kilianza tarehe 31 Machi na kuhitimishwa tarehe 1 Aprili, 2017 katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dodoma.
 Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii, Mhe. Musa Azzan Zungu (Mb) akiongoza majadiliano ya kikao cha Kamati hiyo kilichokutana UDOM Dodoma kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2017/18 kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na taasisi zilizochini ya Wizara hiyo na kupitia Mpango wa bajeti kwa mwaka 2017/18. Wa pili kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy A. Mwalimu akifuatilia mwenendo wa kikao, na kushoto ni Naibu Waziri Mhe. Hamisi A. Kigwangalla (Mb). Kamati imeipongeza Wizara kwa jitihada zinazofanyika katika kutekeleza majukumu ya kisekta na imeridhia Bajeti ya Wizara kwa hatua zinazofuata. 
 Kulia ni Mhe. Hamisi A. Kigwangalla (Mb) akifuatilia kwa makini maelezo ya Mhe. Waziri (Hayupo pichani) kuhusu Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ikiwasilishwa na Mhe. Waziri (Hayupo pichani). Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Idara kuu ya Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba S. Nkinga na kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara Idara kuu ya Afya Dkt.Mpoki Ulisubisya. Wakifuatilia Taarifa inayowasilishwa kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii katika kikao cha siku mbili kilichofanyika Chuo kikuu cha Dodoma na kuhitimishwa leo mchana.
 Kulia ni Katibu Mkuu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Idara kuu ya Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba S. Nkinga, katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara Idara kuu ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya. Wakisikiliza na kunukuu maelezo ya hoja zilizotolewa na wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii katika kikao cha siku mbili kilichofanyika Chuo kikuu cha Dodoma na kuhitimishwa leo mchana. Kushoto ni mmoja wa waheshimiwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jmaii. 
 Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii wakipitia Taarifa za Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto iliyowasilishwa na kujadiliwa kwa muda wa siku mbili katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dodoma na kuhitimishwa leo tarehe 1 Aprili, 2017. Taarifa hiyo imepitishwa kwa  hatua za maandalizi ya vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotarajiwa kuanza mapema mwezi Aprili, 2017. Wengine katika mstari wa nyuma ni Watendaji waandamizi wa Wizara hiyo. Kikao hicho  kilianza Alhamis tarehe 31 Machi na kuhitimishwa tarehe 1 Aprili, 2017 katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dodom
 Baadhi ya waheshimiwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii wakipitia Taarifa za Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto iliyowasilishwa na kujadiliwa kwa muda wa siku mbili katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dodoma na kuhitimishwa leo tarehe 1 Aprili, 2017. Taarifa hiyo ambayo imepitishwa na Kamati kwa maandalizi ya vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotarajiwa kuanza mapema mwezi Aprili, 2017. Wengine katika mstari wa nyuma ni Wakurugenzi waandamizi wa Wizara hiyo. Kikao hicho cha siku mbili kilianza Alhamis tarehe 31 Machi na kuhitimishwa tarehe 1 Aprili, 2017 katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dodoma.
Baadhi ya waheshimiwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii Taarifa za Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto wakipitia maelezo ya Taarifa iliyowasilishwa na kujiaandaa kwa ajili ya majadiliano wakati wa kikao cha siku mbili kilichofanyiaka ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dodoma na kuhitimishwa leo tarehe 1 Aprili, 2017. Taarifa hiyo imepitishwa na Kamati kwa hatua za maandalizi ya vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotarajiwa kuanza mapema mwezi Aprili, 2017. Wengine katika mstari wa nyuma ni Wakurugenzi waandamizi wa Wizara. Kikao hicho kilianza Alhamis tarehe 31 Machi na kuhitimishwa tarehe 1 Aprli, 2017 katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dodoma.

Post a Comment

0 Comments