Kimbunga kiitwacho Irma kimelikumba eneo la Florida huku kikiwa na upepo wenye mwendo wa kasi ya Kilomita 209 kwa saa.
Kimbunga hicho ambacho kimeshauwa watu watatu Florida kimepandishwa daraja na kufikia daraja la 4 kwa ukubwa.
Watu milioni 6.3 wameshambiwa kuondoka kwenye nyumba zao kwa lazima ama kwa hiyari yao ili kuepuka maafa.
Kimbunga hicho tayari kimesababisha vifo vya watu 25 katika eneo la ukanda wa Caribbean tangu kilipoanza mapema wiki hii.
Kimbunga Irma kikiwa kimeuangusha mti ulioangukia gari
Boti likiwa limesukumwa kando na kimbunga Irma









0 Comments