Random Posts

Mtendaji Mkuu wa TFS, Prof. Dos Santos Silayo afanya ziara Wilayani Mkuranga kwa ajili ya kuimarisha uhifadhi na kujadili mikakati ya kuzuia wavamizi kwenye misitu wa hifadhi

 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)  Prof. Dos Santos Silayo kuu akisaini jana kitabu cha wageni  mara alipotembelea ofisi  ya Mkuu wa Wilaya ya  Mkuranga ikiwa  lengo la ziara hiyo  ni kujadili mikakati ya kuzuia wavamizi kwenye msitu wa hifadhi. 
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga  akimuonesha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)  Prof. Dos Santos Silayo  baadhi ya maeneo ya Hifadhi  yaliyovamiwa na kuanzishwa shughuli za kibinadamu katika Hifadhi ya Msitu wa Vikindu. Lengo la ziara Mtendaji Mkuu wa TFS hiyo ilikuwa ni kuimarisha  uhifadhi kwa kujadili mikakati ya kuzuia wavamizi kwenye msitu wa hifadhi.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)  Prof. Dos Santos Silayo akiteta neno na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga wakati wa  ziara ya kujionea jinsi wananchi walivyovamia na kuanzisha shughuli za kibinadamu katika Hifadhi za Msitu wa Vikindu. 
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)  Prof. Dos Santos Silayo alimpomtembelea jana  Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga ofisini kwake akimuonesha  baadhi ya maeneo kwenye ramani jinsi  vyanzo  vya maji vilivyoharibika kutokana na tabia ya baadhi ya wananchi kuvamia kwa kuanzisha shughuli za kibinadamu katika Hifadhi za Misitu. Mwingine ni Meneja  Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania wa Wilaya ya Mkuranga Christina Mohamed .
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)  Prof. Dos Santos Silayo akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga mpaka kati kijiji na Msitu wa Hifadhi ya Vikindu mara baada ya kufanya ziara ya kujionea jinsi wananchi walivyovamia na kuanzisha shughuli za kibinadamu katika Hifadhi za Msitu huo.

Post a Comment

0 Comments