Mhandisi
kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo
maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Liberatha
Alphonce, akielekeza jambo kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya
Nachingwea mkoani Lindi, kuhusu umuhimu wa masomo ya Sayansi na Hesabu.
Wanafunzi
wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya Nachingwea mkoani Lindi, wakimsikiliza
Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi),
Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi.
Liberatha Alphonce (hayupo pichani), alipofika shuleni hapo kuhamasisha umuhimu
wa masomo ya Sayansi na Hesabu.
Maabara
ya Shule ya Sekondari ya wasichana ya Nachingwea mkoani Lindi, licha ya
kukamilika lakini bado inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa vifaa.
Jengo
la maabara la Shule ya Kutwa ya Nachingwea Sekondari, ambalo halijakamilika
kutokana na uhaba wa fedha, hali inayopelekea wanafunzi hushindwa kujifunza
masomo ya sayansi kwa vitendo kutokana na changamoto hiyo.
Wahandisi
kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo
maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, wakisikiliza
maoni kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kilwa, mkoani Lindi (hawapo
pichani), walipofika shuleni hapo kuhamasisha usomaji wa masomo ya Sayansi na
Hesabu kwa wasichana.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano.





0 Comments