Random Posts

MAO WATOA MSAADA WENYE THAMNI YA TAKRIBANI SH. MILIONI 6.

Na Mwandishi Wetu Dar es salaam
Chama Cha Marafiki wa Oljoro (MAO) wametoa msaada wa vitu mbalimbali wenye thamani ya shilingi milioni 6 katika Chama cha Kulea Watoto Mayatima(CHAKUWAMA) kilichopo jijini Dar es salaam.
Akiongea na Waandishi wa habari wakati wa kukabidhi misaada hiyo leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa MAO Bw. Walter Chipeta amesema kuwa wameamua kufanya hivyo ili kuwafariji watoto hao na kuwajengea maisha yenye furaha.
“Tumeamua kuja kutembelea na kutoa misaada kwa watoto wetu waishio katika kituo hiki ili kusaidia kutimiza malengo ya watoto wetu pamoja na kuazimisha kumbukumbu ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere” alisema Bw. Chipeta.
Kwa upande wake Mratibu wa Tukio hilo kutoka MAO Bi. Pamela Lwakabare amesema kuwa  msaada iliyotolewa ni pamoja na Vyakula na matunda,vifaa vya michezo ya watoto,mavazi,vyombo vya chakula ,vifa vya usafi na vinywaji amabvyo vina thamani ya takribani shilingi milioni 6.
Naye katibu Mtendaji wa CHAKUWAMA Bw. Hassan Hamis amesema kuwa anashukuru kwa msada huo kwani imepunguza gharama ya mahitaji kwa watoto  wapatao 64 katika kujikimu kila siku.
Mbali na hayo Mtoto anayeishi katika kituo hiko Nasiim Kasmal (11) amempongeza Rais wa awamu ya tano Dkt. Pombe John Magufuli kwa kuanzisha elimu bure kwani imewarahisishia watoto wanaoishi katika mazingira magumu kupata elimu kwa urahisi 
 Mwenyekiti wa   chama cha Marafiki wa Oljoro (MAO) Bw. Walter Chipeta kushoto akimkabidhi msaada  wa vitu mbalimbali vyenye mahitaji muhimu kwa katibu mtendaji wa Chama cha Kulea Watoto Mayatima (CHAKUWAMA) Bw. Hassan Hamis kulia leo jijini Dar es salaam.
Wanachama wa  chama cha Marafiki wa Oljoro (MAO) wakiwa kwenye picha ya pamoja na baahi ya watoto  wanaoishi katika Chama cha Kulea Watoto Mayatima (CHAKUWAMA) wakati walipotembelea watoto ha oleo jijini Dar es salaam.


Picha na Mpiga Picha wetu.

Post a Comment

0 Comments