Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, QS Albert Munuo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jiji Dar es salaam Oktoba 4, 2017 kuhusiana na maandalizi ya semina endelevu ya bodi ya Usajili wa
wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi itakayofanyika oktoba 12-13 2017
mlimani city jijini Dar es salaam (kulia) Afisa Mkuu Ukaguzi wa Ndani wa Bodi hiyo, Ezekiel Stephen, na kushoto Mwanasheria wa Bodi, Ibrahim Mohamed.
Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, QS Albert Munuo (kushoto katikati) akiendelea kutoa ufafanuzi kuhusiana na maandalizi ya semina endelevu ya bodi ya Usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi itakayofanyika oktoba 12-13 2017 mlimani city jijini Dar es salaam (wakwanza kulia) Afisa Mkuu Usajili wa Bodi hiyo, Mashaka Bundala.
Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, QS Albert Munuo (kulia katikati) akijibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari wakati akielezea kuhusiana na maandalizi ya semina endelevu ya bodi ya Usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi itakayofanyika oktoba 12-13 2017 mlimani city jijini Dar es salaam.
.....
Waziri
wa Ujenzi uchukuzi na mawasiliano professa Makame mbarawa anatarajiwa kuwa
mgeni rasmi kwenye semina endelevu ya bodi ya Usajili wa wabunifu majengo
na wakadiriaji majenzi itakayofanyika oktoba 12-13 2017 mlimani city
jijini Dar es salaam.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kaimu msajili wa bodi hiyo Albert
Munuo amesemakuwa semina hiyo inalenga kuwapa frusa wataalamu katika sekta ya
ujenzi kupata nasaha kutoka Kwa viongozi wa serekali na kubadilishana uzoefu wa
kazi za kitaalamu kwa lengo la kuziboresha.
Aidha
ameongeza kuwa semina hiyo pia itawanoa wabunifu majengo, wasanifu wa
ndani ya majengo, wabunifu wa mandhari ya nje, wakadiriaji majenzi,
wasimamizi ujenzi, watathimini majengo na wadau wengine katika sekta ya ujenzi
ili kukabiliana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia katika sekta ya ujenzi.
Sanjari
na hayo Bw.Munuo amesema semina hiyo itakuwa na mada mbalimbali ikiwemo mbinu
za kupunguza madhara ya matetemeko ya ardhi, ukaguzi wa miradi ya ujenzi pamoja
na matengenezo ya majengo na miundombinu katika sekta ya ujenzi.
Hata
hivyo ametoa wito kwa wadau wa sekta ya ujenzi ikiwemo wahandisi, wakadiriaji
majenzi na wabunifu majengo kuhudhuria kwa wingi kwenye semina hiyo ili
kuongeza ujuzi na maarifa ya kuboresha utendaji kazi wao.
0 Comments