Random Posts

Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania wafanya ziara ya kujione mradi wa kilimo cha papai Ruaha Iringa

Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania wakiwasili Ruaha -Kware Wilya ya Kilolo Mkoa wa Iringa wakati wa ziara ya kujionea shamba lenye ekari 3000 kwaajili ya kuwekeza kilimo cha PAPAI.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita Mkakati wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania, Dkt. Kissui Stephen akielezea malengo ya ziara hiyo (kushoto kwake) Mkurugenzi wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania pia mwanzilishi wa mtandao huo, Adam ngamange, kulia katikati ni Afisa Mtendaji Kilimo na Mifugo wa Ruaha -Kware Wilya ya Kilolo Mkoa wa Iringa, John Mchopa, na Mwenyeji wa Shamba hilo na mkulima wa Ruaha, Amani Matinya.  

Ambapo amesema lengo ya ziara hiyo ni kuwaleta wakulima waweze kuona mashamba wanaotarajia kuanza kulima kwa mkataba pia kutangaza mtandao huo ili watu waanze kuwaza kijani na kila mtu arudi kwenye kilimo.

Alisema kama mtu awezi kulima myenyewe kuna wataalamu mbao watawekwa shambani kwa garama nafuu ambao wataweza kuendeza mashamba hayo.

Pia  Dkt. Kissui alisema wanatumia mbegu za kisasa zinazo zalisha mara tatu zaidi na mbolea za Organic  ambazo hazina madawa na haziharibu aridhi ili kuhakikisha vizazi na vizazi viweze kufurahiya.

Alisema pia wanatanga maswala ya masoko kutokana huu ulimwengu wa masoko yani unaanza kwanza kutafuta masoko ndipo unaanza kulima.
"Sisi tunaanza kutafuta masoko ya ndani na nje na baadaye tunawaaunganisha wakulima kwenye masoko" Alisema Kissui.
Mkurugenzi wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania pia mwanzilishi wa mtandao huo, Adam ngamange akielezea miradi ya kuamasisha kilimo na ufugaji kibiashara wakati wa ziara ya kutembela shamba kwaajili ya kuwekeza kilimo cha PAPAI Ruaha -Kware Wilya ya Kilolo Mkoa wa Iringa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania pia mwanzilishi wa mtandao huo, Adam alisema katika mtandao wanafanya miradi ya uwamasishaji kilimo na ufugaji kibiashara.

Alisema waligundua watanzania wengi wanalima lakini sio kibishara ambapo wameanza na miradi mitano katika miradi hiyo kuna maeneo maalum kama Ruaha ni aridhi yakupata papai iliyokuwa salama kwakuwa watangaza maswala ya kilimo hai.

Aliongeza kuwa mradi huo wenye ekari 384 ambazo watazigawa katika mafungu ya ekari 32 kila ekari ambazo zitapandwa katika utaratibu wa kili mwezi mara moja ili waweze kusamba papai kwenye masoko makubwa.
 Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania wakitembelea na kukagua shamba kwaajili ya kuwekeza kilimo cha PAPAI.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita Mkakati wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania, Dkt. Kissui Stephen akimtambulisha Mwenyeji wa Shamba hilo na mkulima wa Ruaha, Amani Matinya.  
 Mwenyeji wa Shamba hilo na mkulima wa Ruaha (alienyosha mkono), Amani Matinya akiwaonesha wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania ukumbwa shamba hilo na mbinu zinazotumika kumwagilia.
 Muonekano wa shamba hilo.
 Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania wakielekea kujionea maji yanayotoka Mto Lukosi unaotumika kwaajili ya kilimo cha umwagiliaji.
 Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania wakiangalia mashine zinazovuta maji kutoka Mto Lukosi kwajili ya kilimo cha umwagiliaji.
 Muonekano wa Mto Lukosi.
 Mmoja wa wakulima wa eneo la  Ruaha -Kware Wilya ya Kilolo Mkoa wa Iringa(kulia) akifafanua jinsi maji yanavyo sambazwa kwa wakulima.
 Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuhitimisha ziara hiyo.
Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania wakipanda kwenye basi tayari kuanza safari kuelekea jijini Dar es Salaam.

HABARI/ PICHA NA RICHARD MWAIKENDA-KAMANDA WA MATUKIO BLOG

Post a Comment

0 Comments