Random Posts

Maginga Business Holdings Company Ltd yakwamisha ujenzi wa barabara ya Namelock –Sunya

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa kata ya Engusero –Wilayani Kiteto wakati wa ziara yake ya kazi Wilayani hapo.
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo (katikati) akimskiliza Meneja wa TARURA Wilaya ya Kiteto Eng.Gerald Matindi akielezea hali ya ujenzi wa barabara ya Namelock-Sunya.a
   Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(kwanza kushoto) akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magesa, Mbunge wa Kiteto Mhe.Emanuel Papiyani na Mwenyekiti wa Ccm Wilaya wakikagua ujenzi wa barabara ya Namelock –Sunya eneo linalojengwa na Mkandarasi Maginga Business Holdings Company Ltd ya mjini Dodoma.
 Muonekano wa barabara ya Namelock –Sunya eneo linalojengwa na Mkandarasi Maginga Business Holdings Company Ltd ya mjini Dodoma ambaye yuko site kwa  miezi minne sasa lakini hali ya ujenzi wa barabara hiyo ikiwa hairidhishi.


Nteghenjwa hosseah, Kiteto

Kampuni ya Maginga Constraction ya mjini Dodoma iliyopewa kandarasi ya ujenzi wa barabara ya Namelock – Loltepes-Sunya Wilayani Kiteto kwa kiwango cha lami imekwamisha mradi huo kwa kutofanya kazi zilizoainishwa kwenye mkataba kwa kipindi cha miezi minne baada ya kukabidhiwa kazi hiyo.

Akikagua barabara hiyo wakati wa ziara ya kikazi Wilayani humo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo ametoa siku kumi na nne kwa Mkandarasi huyo kukamilisha kazi au kurejesha kazi hiyo  kwa Wakala wa barabara za mijini na Vijijini (TARURA) ili apewe  Mkandarasi mwingine atakayeweza kwenda na muda uliyoainishwa kwenye mkataba.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Waziri Jafo amesema tar 17/10/2017 nitakuja tena hapa kuangalia maendeleo ya mradi huu; Mkandarasi huyu afanyiwe tathmini ya haraka  kama ana uwezo wa kufanya kazi hii ama lah msitishe mkataba wake kwa sababu mpaka sasa hivi amekwishatumia nusu ya muda aliyopewa lakini alichofanya hakielewi na barabara hii ni muhimu kwa matumizi ya wananchi haswa wakulima ambao hutumia barabara hii kusafirisha mazao yao toka shambani hadi Sokoni.

“Siwezi kuvumilia wananchi wangu wapate tabu kwa sababu ya uzembe wa mkandarasi ninaagiza mambo matatu, Mkandarasi aondolewe haraka na apatiwe atakayeweza kufanya hii kazi ama  kazi zilizoainishwa kufanyaika katika kipindi cha miezi mine zionekane zikiwa kwenye ubora au tumuondoe Meneja wa Tarura Wilaya ya Kiteto na tumlete atakayeweza kusimamia miradi kwa ufanisi”aliongeza Mhe.Jaffo.

Akielezea hali ya mradi Mbunge wa Kiteto Mhe.Emanuel Papian amesema haridhishwi na utendaji kazi wa mkandarasi Maginga Hoding Cooperation kutokana na uzembe anauofanya kwenye mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya Namelock-Sunya yenye urefu wa Km 44 na amekwisha mlalamikia mara kadhaa kwenye uongozi wa Wilaya pamoja na TARURA lakini haoni hatua stahiki zikichukuliwa dhidi yake.

“Mradi huu walipewa wakandarasi wawili mmoja akiwa huyu Maginga ambaye anatakiwa kujenga barabara ya urefu wa Km 44 ambaye anajenga kuanzia namelock mpaka Loltepes ambae namlalamikia leo hii na Mkandarasi mwingine  ni Deniko Constraction ambaye naye anajenga Km 44 kuanzia Loltepes mpaka Sunya lakini yeye ameshafanya kazi kubwa na yenye ubora; Sasa nashangaa kwanini huyu Maginga yeye hafanyi na hachukuliwi hatua yeyote ninaomba Mhe.Waziri uingilie kati suala hili” alisema Mhe.Papian.

Naye Meneja wa Wilaya ya Kiteto Mhandisi Gerald Matindi amesema changamoto hiyo walikwishaibaini na kumuandikia Mkandarasi Maginga barua ya kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo na wanaendelea na kufuatilia na endapo watathibitisha hawezi kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo watasistisha mkataba wake mara moja.

Mradi wa ujenzi wa barabara ya  Namelock – Loltepes-Sunya inajengwa kwa urefu wa Km 88 ambapo wakarasi wawili Maginda constraction pamoja na Deniko Constractio wamepewa kazi ya kujenga kila Km 44 kila mmoja na kazi zilizoainsha ni pamoja na ujenzi wa madaraja, makalavat, mifereji ya kusafirishia maji ya mvua pamoja na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha changarawe.

Kazi hii inatarajiwa kukamilika mwezi March,2018 na itagharimu Fedha za kitanzania zaidi ya shilingi Bil 7 ambazo ni Fedha za ruzuku “Feed for Future” ikiwa ni msaada kutoka katika Serikali ya Watu wa Marekani “USAID: Fedha hizi hujenga barabara kwenye halmashauri zenye mazao mengi ili kurahisisha usafirishaji wa mazao kutoka shambani hadi Sokoni.

Post a Comment

0 Comments