Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangallaakitoa maagizo kwa uongozi wa bandari ya TPA.
Baadhi ya magogo hayo yaliyokutwa katika makontena bandarini hapo
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla wakiwa katika eneo la bandari ya nchi kavu ya Malawi Cargo. wakati wa kukagua magogo hayo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua baadhi ya mbao zilizokutwa bandarini hapo katika eneo la Malawi Cargo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua baadhi ya mbao zilizokutwa bandarini hapo katika eneo la Malawi Cargo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akionyeshwa nyaraka ya idadi ya makontena katika eneo la Malawi Cargo.
Zoezi la ukaguaji likiendelea.
Baadhi ya magogo yaliyokutwa bandarini hapo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi
Kigwangalla (MB) ametoa mud wa siku 30 kwa wahusika ambao ni wamiliki wa magogo
yaliyokamatwa katika bandari ya Dar e s Salaam (TPA) ambayo yalikuwa
yasafirishwe nje ya Nchi, kujitokeza haraka kueleza wameyato wapi na walikuwa
na lengo gani baada ya kuyatelekeza bandarini hapo kwa muda wa miaka 10
sasa huku mengine yakitelekezwa pasipo kuwa na vibali maalum.
Dk.Kigwangalla ametoa kauli hiyo
baada ya kufanya ziara ya ghafla bandarini hapo kukagua mali na bidhaa
zinazoshughulikiwa na Wizara yake hiyo ambapo katika zkukagua kwake huko
alibaini uwepo wa makontena hayo 55 ambayo yapo kwa miaka 10 sasa yakihifadhiwa
huku wahusika wakishindwa kujitokeza.
“Naagiza mamlaka zilizo chini ya
wizara yangu kuhakikisha wanahakiki magogo yote yalipo hapa bandarini. Mwenye
huu mzigo lazima ajulikane hasa haya magogo 938, Ndani ya siku 30 mwenye haya
magogo atangaziwe na ajitokeze vinginevyo itabaki kuwa mali ya Serikali”
alisema Dk. Kigwangalla.
Hata hivyo aliagiza pia kontena
55 zilizokutwa bandarini hapo zenye magogo pia nazo wahusika wajitokeze na
nyaraka zao kamili ili waeleze kama kweli wameyatoa Zambia magogo hayo
ama sehemu gani hivyo wajitokeze na wasipofanya hivyo ndani ya siku hizo 30,
magogo hayo yatataifishwa na kuwa mali ya Serikali.
Katika ziara hiyo, Waziri
Dk.Kigwangalla aliweza kutembelea bandari ya Dar es Salaam pamoja na maeneo
yanayohifadhiwa magogo hayo zikiwemo bandatri ya nchi kavu ya NASACO, Malawi
(Malawi Cargo) na baadae eneo hilo la bandari ya Dar es Salaam.
Akiwa katika eneo la Malawi Cargo, Waziri Dk.
Kigwangalla aliweza kushuhudia makontena mbalimbali yakiwemo yale ya mbao
aina ya mitiki ambayo inatarajiwa kusafirishwa nje ya nchi huku akibaini uwepo
mkubwa wa udanganyifu kwa wasimamizi wa upakuaji na usafirishaji katika eneo
hilo la bandari ambao awali walitaja idadi ndogo ya makontena ya mbao mbele ya
Waziri hali iliyopelekea kuanza kuyakagua makontena yote ndani ya eneo hilo











0 Comments