Random Posts

Uchaguzi mkuu wa shimiwi kufanyika Desemba 16,2017 mkoani Morogoro

YAH: UCHAGUZI MKUU WA SHIMIWI
Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) linatarajia kufanya  Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Shirikisho tarehe 16 Desemba, 2017 katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Mount Uluguru Mkoani Morogoro. Kwa mujibu wa Sura ya III Ibara ya 15 (2) ya Katiba ya SHIMIWI Wajumbe wa Mkutano huu ni wenyeviti wa Vilabu, Makatibu wa Vilabu na mjumbe mmoja aliyechaguliwa na Klabu kuwakilisha katika Mkutano Mkuu wa SHIMIWI.
Aidha, Sura ya VII Ibara ya 38.1 (i- viii) ya Katiba Mkutano huu utawachagua Viongozi wafuatao;  
  1. Mwenyekiti   2. Makamu Mwenyekiti  3. Katibu Mkuu  4. Naibu Katibu Mkuu
  1. Mweka Hazina  6. Mweka Hazina Msaidizi 7. Wajumbe watano (5) wa Kamati ya Utendaji   8. Wajumbe wawili (2) wa viti maalum Wanawake.
Baraza la Michezo la Taifa (BMT) wenye mamlaka ya kusimamia Uchaguzi huu tayari wameshatangaza nafasi hizo.

Hivyo, nawaomba watumishi tujitokeze kugombea nafasi hizo pia waajiri kuwawezesha viongozi waliotajwa katika para ya kwanza hapo juu wahudhurie katika Mkutano huu. Kiongozi atakayeshindwa kuhudhuria Mkutano anapaswa kuwasilisha taarifa itakayoeleza sababu za kutohudhuria ili Mkutano utoe maamuzi na endapo zitakuwa nje ya uwezo wa Mkutano zitafikishwa kwa Mlezi wa Shirikisho ambaye ni Katibu Mkuu Kiongozi na Mkuu wa Utumishi wa Umma.

Shirikisho linasikitishwa na taarifa zinazotolewa na baadhi ya Watumishi kuwa SHIMIWI imefutwa. Kwa taarifa hii nawajulisha Watumishi wote wa Serikali kuwa SHIMIWI bado ipo na inaendelea na shughuli zake kama kawaida. 

Tunawaomba viongozi kuendelea kusimamia shughuli za Michezo katika maeneo yao ya Kazi ili kulinda na kuimarisha afya za Watumishi.
Moshi Y. Makuka

KAIMU KATIBU MKUU – SHIMIWI

0754 – 763140          Imetolewa leo Tarehe 12 Desemba, 2017

Post a Comment

0 Comments