Waziri
wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina (mwenye miwani na kofia
)akisikiliza
jambo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Ukerewe, Frank
Bahati (kushoto) wakiwa kwenye boti ya doria kutoka katika kijiji Kakukuru
wakielekea kwenye kambi ya uvuvi ya Kisiwa cha Galinzila ambapo
Mhe.Waziri alifanya mkutano na wavuvi . Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe
Estomiah Chang’a. (Na John Mapepele)
Mmliki wa ghala
lenye shehena ya marobota 600 ya nyavu haramu
za kuvulia samaki zisizoruhusiwa kisheria zenye thamani ya shilingi
milioni mia tano, Meshaki Chacha akihojiwa na Mwandishi
wa Habari wa ITV baada kikosi kazi kilichoundwa na Waziri wa Mifugo
na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina(mwenye kofia) kuvamia ghala lake lililopo
jijini Mwanza leo. Ametakiwa kulipa faini ya shilingi milioni
50 ndani ya masaa 24 leo. (Na John Mapepele)
- Aapa kutokomeza uvuvi haramu nchini
- Asema imebaki 3% tu ya Sangara wanaokubalika kuvuliwa katika ziwa Victoria
Na
John Mapepele
Waziri wa Mifugo na
Uvuvi, Mhe Luhaga Joelson Mpina amekamata marobota 1152
ya aina mbalimbali za nyavu haramu zisizoruhusiwa kisheria
kutumika kuvulia samaki zenye thamani ya shilingi milioni 894
jijini Mwanza na Singida ambapo baadhi ya nyavu hizo zimetaifishwa
na nyingine kuteketezwa na wamiliki wakitakiwa kulipa faini ya
shilingi milioni 120 ndani ya masaa 24 kwa makosa ya kufanya biashara
ya nyavu hizo kinyume cha sheria.
Akiongea na Vyombo
vya Habari jijini Mwanza katika ghala la nyavu la Meshack Chacha
mara baada ya kukamata shehena ya marobota 600 ya nyavu haramu
kwenye ghala lake, Mhe. Mpina alisema nyavu haramu 294 kati ya 894 zilikamatwa
na kikosi kazi maalum cha kudhibiti uvuvi haramu katika kanda ya Ziwa
Victoria alichokiunda hivi karibuni wakati mmoja wa wafanyabiashara
hao Masagati Majani alijaribu kutorosha vyavu hizo kwa kutumia gari
aina ya Scania lenye namba za usajili T.452 BBS kutoka Mwanza kuelekea
Dar es Salaam.
Gari hilo lipo katika
kituo cha polisi cha Singida kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria ambapo
kulingana na sheria ya Uvuvi namba 22 ya mwaka 2003, imetoa
mamlaka kwa watendaji wa Serikali kutaifisha mali zote zilitumika katika
uvuvi haramu kupitia kifungu cha 37(a) (ii) na (iii)
Aliwataja wamiliki wengine
ambao walikamatwa kutokana na kujihusisha na biashara haramu ya
uagizaji na uuzaji wa vyavu zisizoruhusiwa kisheria kuwa ni Josia Jonam
Obielo, Jeremiah Asam na Dastun Venant ambapo alisema Serikali imejipanga
kuhakikisha kwamba wafanyabiashara wote wanao agiza
na kuuza zana haramu za uvuvi wanakamatwa na sheria kali zinachukuliwa
ili kudhibiti uvuvi haramu nchini.
“Niliapa kusimamia
ulinzi wa raslimali za uvuvi nchini hivyo nitahakikisha operesheni
hii inakuwa ya kudumu katika kupambana na uvuvi haramu hadi uvuvi
haramu utakapokwisha” alisisitiza Mpina
Katika hatua nyingine
Waziri Mpina amelaani kitendo Kiwanda cha Sunflag cha mkoani
Arusha kwa kuendelea kufadhili uvuvi haramu nchini kutengeneza na
kuuza
vyavu za kuvulia samaki zisizoruhusiwa kisheria wakati Serikali imekuwa
ikisisitiza viwanda vyote nchini kuacha tabia ya kufadhili uvuvi haramu
kwa kutengeneza zana haramu za uvuvi.
Waziri Mpina ameagiza
watalam kwenda mara moja katika kiwanda hicho kuchunguza ukweli
wa jambo hilo ili sheria zichukue mkondo wake.
Hivi karibuni Waziri
Mpina aliunda Kikosi maalum cha kupambana na uvuvi haramu ambapo katika
kipindi kisichozidi siku kumi na nne zaidi ya zana haramu za uvuvi ikiwa
ni pamoja na nyavu zenye jumla ya bilioni tatu zimeteketezwa katika
kanda ya ziwa Victoria peke yake huku viwanda vitano vya kusindika
samaki vilivyopo jijini Mwanza vikitakiwa kulipa jumla ya shilingi milioni
180 ndani ya masaa 24.
Viwanda hivyo vilitozwa
faini hiyo kutokana na kuendelea kuwa wafadhili wakuu wa uvuvi haramu
kwa kununua na kuchakata samaki aina Sangara wachanga na wazazi kinyume
cha Sheria ya Uvuvi.
Waziri Mpina alisema
Sheria ya Uvuvi namba 22 ya Mwaka 2003 na Kanuni zake za mwaka
2009 kifungu cha 90(1) inataka samaki wanaovuliwa waandaliwe katika
mazingira yanayokidhi vigezo vya usalama kwa mlaji na kwamba
ni kosa kisheria kuwavua au kuchakata samaki aina ya Sangara walio chini
ya sentimeta 50 kwa kuwa ni wachanga na sentimita 25kwa Samaki aina
ya Sato. Pia sentimita 85 kwa Sangara kwa kuwa ni wazazi wanaotakiwa
kundelea kuzaa.
Waziri Mpina alisema samaki
aina ya Sangara kwenye
Ziwa Victoria wapo katika hatari ya kutoweka kabisa katika kipindi cha
miaka miwili endapo hali ya uvuvi haramu ukiachwa uendelee bila
kuchukua hatua za haraka na madhubuti kudhibiti janga
hili.
Alisema kulingana na
utafiti uliofanywa na
Taasisi ya Utafiti wa Samaki Tanzania (TAFIRI) 2017 unaonesha kuwa samaki
wachanga waliochini ya sentimita 50 wasioruhusiwa kuvuliwa ni asilimia
96.6 , samaki wazazi walio zaidi ya sentimita 85 ambao pia hawarusiwi
kuvuliwa ni asilimia 0.4 na samaki wa sentimita 50 mpaka 85 ambao ndio
wanafaa kuvuliwa ni asilimia 3 tu hivyo juhudi za pamoja za wadau wote
wa sekta ya uvuvi zinahitajika ili kurejesha raslimali ya uvuvi katika
Ziwa Victoria kwa faida ya vizazi vya sasa na baadaye.




0 Comments