TECNO
kampuni ya simu za mkononi iliyojizolea umaarufu barani Africa na Mashariki ya
kati kupitia uzalishaji wake wa simu janja (smart phone) imeendelea kushika
chati katika masoko mbalimbali barani Afrika.
Kama
ilivyo kwa kila mwaka, kampuni ya TECNO huzindua simu mpya na hua ni muendelezo
wa matoleo yaliopita.
Kwa mwaka huu TECNO wanaachilia simu ikiwa ni muendelezo
wa simu aina ya CAMON. Camon imekua moja wapo ya simu janja (smartphone) pendwa
sana kwa wadau kwa mwaka 2017!
Wanatarajia
kuachilia simu hio ndani ya miezi ya kwanza (Januari – March) mwaka huu na
itakua ni simu ya kipekee kwani itakua na vigezo maalumu kulinganisha na simu
zingine zilizopita kabla!
Kadri
miaka inavyosogea na kuendelea teknolojia ya simu, miundo ya simu, vigezo,
mahitaji na matumizi ya simu hubadilika na kuongezeka, hivyo kama kampuni
imekua ni jambo muhimu kuweza kutoa simu zinazokidhi mahitaji ya wadau na
watumiaji wa bidha zake hivyo kutoa toleo jipya kabisa!
Je, ni
simu gani na itakua na vigezo/muundo gani?
Fuatilia
kurasa za TECNO katika mitandao ya kijamii na tovuti yao kujua zaidi!
0 Comments