Mtazamo News--
KUNDI la The Mafik linaloimba muziki wa aina
mbalimbali limezinduliwa juzi usiku huku wasanii watatu wanaounda kundi hilo
wakiahidi kuleta mabadiliko katika tasnia ya muziki hapa nchini hasa muziki wa
kundi
Wasanii wanaounda kundi hilo ni Rhino, Hamadai na
Mbalamwezi ambao wote ni wasanii wa muziki wa dansi pia kwa kuwa wametokea
kwenye bendi ya The Mafik Band inayopiga kila Jumapili klabu ya Next Door
Oyster bay, Dar es Salaam.
Akizungumzia ujio wa kundi hilo, Meneja wa kundi,
Michael Mlingwa (Mx Carter) aliweka wazi kuwa kundi hilo hadi sasa lina nyimbo
tano ambazo pia video zake zimerekodiwa nchini Afrika Kusini.
Alisema, kwa hiyo juzi wametambulisha wimbo wao
mmoja uitwao Passenger ambao unaingia rasmi sokoni leo huku ukiwa
ummeshatengenezewa video yake pia.
Alisema, wasanii wa kundi hilo wanaweza kuimba kila
aina ya wimbo kwa kuwa ni wasanii ambao wamekulia kwenye muziki na wamekuwa
wakifanya muziki hasa wa bendi kwa muda mrefu.
Alisema" vijana hawa watakuwa wakifanya kazi
kama wasanii watatu kwa pamoja na watakuwa wakiimba muziki wa kawaida na hata
kwa bendi inategemea na uhitaji wa mteja lakini ni wasanii ambao wamekuja
kufanya makubwa kwenye fani hii".
Majina ya wasanii wa kundi hilo ni Salehe Hussein(
Rhino King) Mohamed Mkumba( Hamadai) na Abdallah Yusuph (Mbalamwezi) ambapo
Mbalamwezi aliwaambia wapenzi wa muziki nchini kutarajia kupata burudani safi
ya muziki.
"Hili ni kundi jipya lakini kwa maana ya
tunaoliunda ni wanamuziki wa muda mrefu kwenye medani hii ya muziki hapa
nchini, tumekuwa kwenye bendi na kwa sasa tunasimama kama wasanii wa kundi
ambao pia tupo kwenye bendi"
Kundi jipya la muziki liitwalo The Mafik Band.
Meneja wa msanii wa muziki Shetta, Mx Carter
akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utambulisho wa Kundi jipya la
muziki liitwalo The Mafik Band' uliofanyika katika Club Next Door Masaki Dar es
salaam .
Shetta akizungumza.
Msanii wa kundi la The Mafiq, Salehe Hussein (Rhino King) akiimba kwenye uzinduzi wa
kundi hilo jana kwenye klabu Next Door kulia kwake ni Mohamed Mkumba( Hamadai)
wakati kulia ni Abdallah Yusuph (Mbalamwezi)
Wadau wakishuudia uzinduzi huo.









0 Comments