Random Posts

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Yatembelea na Kukagua Miradi Mbali Mbali Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi.

 Mkuu wa Magereza Mkoa wa Lindi, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Ndg. Rajab Bakari (kushoto) akifafanua jambo pale kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama ilipokuwa inakagua miradi mbali mbali na ukarabati wa mabweni ya wafungwa leo tarehe 17 Machi, 2018 Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi. Katikati ni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Mussa Zungu
 Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kulia) wakati alipowasili kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali na ukarabati wa mabweni ya wafungwa leo tarehe 17 Machi, 2018 Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi.
 Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Cosato Chumi akizungumza wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Lindi katika kikao kilichofanyika leo tarehe 17 Machi, 2018 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akizungumza wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Lindi katika kikao kilichofanyika leo tarehe 17 Machi, 2018 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akizungumza na Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Lindi katika kikao kilichofanyika leo tarehe 17 Machi, 2018 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Post a Comment

0 Comments